Friday, September 22, 2017

DC, KILWA" AZIPIGIA MAGOTI TAASISI ZA FEDHA ZIWAHURUMIE WENYE VIPATO VIDOGO

Na.Ahmad Mmow. 
LICHA ya kuhaidi kuvitafutia mikopo vikundi wajasirimali vilivyopo katika wilaya yake. Mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoa wa Lindi,Christopher Ngubiagai ametoa wito kwa taasisi za fedha zinazotoa mikopo  kuwahurumia watu wenye vipato vidogo kwa kulegeza masharti na kupunguza viwango vya riba. 

Ngubiagai anaetambulika kwa jina la Komredi alitoa wito huo wakati anafungua semina ya wajasiriamali iliyofanyika leo katika mamlaka ya mji mdogo wa Kilwa Masoko.Semina ambayo iliandaliwa na mamlaka ya mapato nchini (TRA) mkoa wa Lindi. 

Alisema tasisi za fedha zinanafasi na uwezo mkubwa wakuisaidia serikali katika mkakati wake wa kuwainua wananchi wake wenye vipato vidogo ili waweze kushiriki kikamilifu ujenzi wa uchumi wa nchi kwa kulegeza baadhi ya masharti na viwango vya riba. 

Mkuu huyo wa wilaya huku akionesha kuhuzunishwa na kuguswa na changamoto wanazokutananazo wajasiriamali,alisema kutokana na masharti magumu na viwango vya riba vilivyopo kwenye baadhi ya benki zinasababisha wakopaji kukosa amani na kuishi kwa hofu badala ya kufurahia mikopo wanayokopeshwa. 

"Zipo taasisi na benki chache ambazo siwezi kuzitaja,zinamasharti na riba nafuu.Lakini ziponyingine ambazo pia sitazitaja,ukikopa unakosa amani,unakosa furaha na unakonda kama unanyonywa damu na jini.Siwezi kuziagiza zilege masharti na riba bali ziwahurumie wenyevipato vidogo," Komredi Ngubiagai aliomba na kusisitiza kwa njia ya utani. 

Kuhusu azima ya kuvitafutia mikopo vikundi vya ujasiriamali,mkuu huyo wa wilaya alisema kwanafasi yake atahakikisha vinapata mikopo kutoka kwenye taasisi za fedha zenye masharti na riba nafuu.Huku akiwahakikishia wajasiriamali hao kwamba taasisi hizo zipo na ameanza kufanyanazo mazungumzo kuhusu hilo.

Mbali na hayo,alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kupokea na kuyafanyia kazi mabadiliko,badala ya kusubiri madiliko yawabadidishe.Ikiwemo kuwa na malengo mahususi katika shuguli zao. 
" Katika dunia ya leo huwezi kufanya shuguli yoyote bila elimu ukatarajia mafanikio.Hata hivyo sekta isiyorasimi inamchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi yoyote duniani,hakuna serikali iliyoweza kuwaajiri wananchi wake wote.Nawaagiza maofisa maendeleo wapeni mafunzo," alisema. 

Kwa upande wake ofisa wa TRA wa kitengo cha elimu kwa walipa kodi wa mkoa wa Lindi,Odupoi Papaa,licha ya kueleza mikakati ya serikali ya kuwainua wafanyabiashara wadogo.Ikiwamo kuzifanyia marekebisho baadhi ya sheria za kodi. 

Aliwaasa wafanyabiashara na wananchi kwa jumla kupeleka malalamiko na ushauri kwenye ofisi zacmamlaka hiyo ili yafanyiwe kazi. 

Habari Ahmed: Alisema mamlaka hiyo  ipo kwaajili ya kuwahudumia wananchi.Kwasababu nitaasisi ya serikali ya wananchi wenyewe.Hivyo maofisa wa idara hiyo niwatumishi wao.

MAWAKILI WA UINGEREZA WAMTAKA MAGUFULI KUANZISHA UCHUNGUZI KUHUSU LISSU

Chama cha mawakili na watetezi wa haki za kibinaadamu nchini Uingereza wamemuandikia barua rais John Pombe Magufuli kikimtaka kuanzisha uchunguzi ulio huru mara moja kuhusu jaribio la mauaji lililotekelezwa dhidi ya mbunge wa Singida mashariki Tundu Lissu. 

Wakili huyo ambaye pia ni rais wa chama cha mawakili nchini Tanzania TLS mnamo tarehe 7 mwezi Septemba alipigwa risasi tumboni na miguuni na watu wasiojulikana katika makaazi yake ya Dodoma. 

''Ufyatulianaji huo wa risasi na maswala mengine ambaye yemetokeo yanayowahusisha mawakili yanatia wasiwasi''. 

Ni muhimu mkubwa kwamba chama cha mawakili kinaheshimiwa kwa kuwa ni kitengo muhimu katika kuhakikisha kuwa sheria zinafuatwa kikamilifu, ilisema barua hiyo. 

Barua hiyo ilisainiwa siku ya Jumatano na rais wa chama cha mawakili Joe Egan ,mwenyekiti wa baraza hilo Andrew Langdon na Mmwenyekiti wake Kirsty Brimelow. 

Mawakili hao wamemwambia rais Magufuli pia kuanzisha uchunguzi kuhusu visa vyengine vya uhalifu vinavyotekelezwa dhidi ya mawakili. 

Visa hivyo ni pamoja na mlipuko katika afisi ya mawakili ya IMMMA chini ya mwezi mmoja na tisho la waziri wa maswala ya kikatiba na sheria Harrison Mwakyembe la kutaka kufutilia mbali chama cha mawakili nchini Tanzania katika kipindi cha miezi saba iliopita. 

Tuesday, September 19, 2017

SABABU TISA ZA KIAFYA KWANINI UNATAKIWA KUTUMIA ZABIBU KILA WAKATI


Kwa mujibu wa tafiti za kiafya zinaonyesha, ipo faida kubwa sana kwa mtu yeyote anayetumia zabibu katika upande wa afya yake. 

Inaonyesha moja kwa moja, zabibu kutokana na wingi wa madini zilizonayo ndani yake, zina uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali kama zikitumiwa kwa uhakika. katika makala haya tumekuwekea dondoo za kukusaidia kukuonyesha baadhi ya magonjwa yanaweza kutibiwa au kuepukwa hasa kutokana na matumizi ya zabibu. 

1. Zabibu inatibu pumu (Asthma) 
2. Zabibu ina imarisha mifupa. 
3. Zabibu inazuia magonjwa mengi ya moyo. 
4. Zabibu inapunguza unene kwa sehemu. 
5. Zabibu inapunguza kisukari. 
6. Zabibu ni kinga ya magonjwa ya meno. 
7. Zabibu ni kinga kwa kansa ya matiti. 
8. Zabibu inapunguza ugonjwa wa mapafu. 
9. Zabibu inapunguza tatizo la kushindwa kuona mbali.

ZALISHA MATANGO UBORESHE KIPATO KWA MUDA MFUPI


Hili ni zao la biashara, pia chakula. Zao hili hustawi na kulimwa kwa wingi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Pwani. 

Matumizi:   Matango hutumika kama tunda, ijapokuwa ni aina ya mboga na huongeza vitamin A, C na maji mwilini. Pia, tango linaweza kutumiwa kama saladi wakati wa mlo. 

Hali ya hewa:  Matango hustawi kwenye hali ya joto, hali kadhali kwenye sehemu yenye joto kidogo pia hustawi. Matango yanahitaji joto wastani wa nyuzi joto 20°C – 25°C. Zao hili pia huhitaji maji kwa wingi, ingawa unyevu ukizidi husababisha magonjwa kwenye majani na maua. 

Udongo:   Kwa ustawi mzuri wa matango, udongo unatakiwa kuwa na rutuba ya kutosha, na chachu ya kuanzia 5.5 hadi 6.7, mwinuko unaotakiwa ni kuanzia mita 1000-1200 kutoka usawa wa bahari. 

Tofauti na ilivyo mazao mengine, matango hayahitaji mwanga mkali sana kwa kuwa husababisha maua dume kuzaliwa, hivyo kuathiri uzalishaji wa idadi ya matunda ya matango. Mwanga kidogo husababisha maua jike kuchanua kwa wingi kuongeza kiwango cha mazao. Mwanga unapokuwa mwingi, inabidi kutumia neti au aina nyingine ya vizuizi ili kupunguza mwanga, ambapo pia itasaidia kulinda mmea dhidi ya upepo mkali ambao unaweza kuharibu maua na matunda, au mmea kwa ujumla. 

Kupanda:  Mara nyingi matango hupandwa moja kwa moja shambani. Wakulima wengine hupanda kwenye vitalu au makopo na baadae kuhamishia miche inapofikia sentimita 8-12. Endapo mbegu zimepandwa shambani moja kwa moja, inatakiwa ipunguzwe na kubakia mche mmoja tu kwenye kila shimo. 

Nafasi:  Nafasi kati ya mche na mche ni sentimita 60-70, na nafasi kati mstari na mstari ni sentimita 70-90. Mimea inatakiwa iwekewe miti ili iweze kuzaa matunda mengi na kuepuka kukaa chini ambapo matunda yanaweza kuoza au kuharibiwa na wadudu. 

Mbolea:   Mbolea ni muhimu sana, kabla ya kupanda au kuhamisha miche. Mbolea inayoweza kutumika ni samadi au ya viwandani isiyokuwa na madhara kwa mazingira na afya ya binadamu. Baada ya kupanda, tumia mbolea ya maji maji kila baada ya siku 14-21, mpaka mmea uweke matunda. 

Palizi:  Palizi ni muhimu , ili kuepuka magonjwa na kunyang’anyana chakula kati ya zao na magugu. 

Wadudu waharibifu:  Wadudu waharibifu wa matango ni pamoja na Vidukari, inzi weupe, na minyoo ya mizizi. 

Magonjwa:  Magonjwa yaliyozoeleka kushambulia matango ni pamoja na Ukungu, fusari, na magonjwa ya virusi. 

Kuvuna:   Matango yanaweza kuwa tayari kuvunwa kuanzia siku 50-60 na matunda yanatakiwa yawe na urefu wa sentimita 15 mpaka 20. Makadirio ya mavuno ni tani 6 kwa ekari moja.

WEKA PEMBENI TABIA HIZI, UJENGE MAISHA YA MAFANIKIO UNAYOYATAKA


Je, uko tayari kufanikiwa kwa namna yoyote ile? Je, kuna changamoto unazopitia na zinakuzuia kufanikiwa, ingawa wewe kiu yako ni kutaka kuona mafanikio yakiwa kwenye maisha yako? Endapo utamuuliza mtu yeyote swali hili, wengi sana watakwambia, ndio wanataka kufanikiwa, tena utajibiwa kwa haraka sana. 

Lakini hata hivyo ni kweli, karibu kila mtu katika maisha yake ana kiu ya kufanikiwa lakini si kila mtu anajua jinsi ya kufanya ili kufanikiwa. Kuna vitabu vingi vimeandikiwa, na makala nyingi zimeandikwa zikieleza kwa wazi nini unapaswa kufanya ili kufanikiwa, na nini ambacho unatakiwa kuepuka sana ili kufanikiwa. 

Pamoja na wingi wote wa vitabu na makala hizo za mafanikio, lakini bado watu hawafanikiwi, wamekuwa ni watu wa maisha yale yale, mpaka unaweza ukaa chini ukajiuliza hivi, shida kubwa ipo wapi? Leo kupitia makala haya, nataka nikukumbushe kwa kifupi sana, baadhi ya tabia unazotakiwa uziweke pembeni ili ufanikiwe. 

Zifuatazo ni baadhi ya tabia ambazo  

1. Ubinafsi. 
Sumu mojawapo kubwa katika biashara na mafanikio kwa ujumla ni ubinafsi. Haitakiwi kuwa mbinafsi unapokuwa kwenye biashara, inatakiwa kutoa ushirikiano na kwa wengine ili mafanikio yako ya kibiashara yaweze kukua. Ukiwa mbinafsi, utakosa ushirikiano kwa wengine na utakwama. 

2. Hofu. 
Hutaweza pia kufanikiwa kama kila wakati kama una hofu kubwa kwenye kila kitu unachotaka kukifanya. Hofu zako zote ulizonazo, zitupe kule. Hofu ni sumu na kizuizi kikubwa sana cha mafanikio yako. Hata hivyo kila mtu ana hofu, lakini hofu zako pia unatakiwa kuzishinda hadi kuchukua hatua kwenye ndoto zako. 

3. Uvivu 
Je, umeshawahi kukutokea asubuhi ambapo kunapokucha unakuwa unajishauri uamke au usiamke, ndani yako kuna kuwa na mabishano mengi sana ya nini ufanye? Kama hali hiyo ilishawahi kukutokea basi ni dalili mojawapo ya uvivu, ambapo ni kitu kimojawapo unachotakiwa kukitupa kule ili uweze kufanikiwa. 

4. Hisia hasi. 
Kuendelea kuwa na hisia hasi, wakati unatafuta mafanikio, huko ni kujitafutia balaa la kushindwa kwenye maisha yako. Hisia hasi ni mbaya katika biashara yako, hisia hasi ni mbaya katika maisha yako pia. Zinakufanya ushindwe kufanya mambo yako kwa ufasaha nakujiona kuwa ni mtu kama wa visasi, ziepuke hisia hizi ili ufanikiwe. 

5. Waepuke watu hasi sana. 
Kama unataka kuwa na mafanikio, epuka sana watu hasi, watu ambao wanaweza kuwa sumu kubwa kwenye maisha yako. Watu hawa hawawezi kukusaidia kitu chochote zaidi watakurudisha nyuma kutokana na maneno yao, kutokana na hisia  zao. Wakimbie watu hawa ili utengeneze mafanikio yako.

MGOGORO GEITA NGOMA BADO TETE

Mgogoro kati ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) na baraza la madiwani wa halmashauri mbili za Geita umechukua sura mpya, baada ya kikao cha kutafuta suluhu kukwama kutokana na mahudhurio hafifu.

Septemba 14, uongozi wa Mkoa wa Geita uliwataka madiwani waliofunga barabara za kuingia GGM kuwa watulivu kusubiri kikao na kamishna wa madini.

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Herman Kapufi alisema wamekubaliana kuahirisha kikao hicho hadi madiwani wanaoshikiliwa polisi watakapofikishwa mahakamani na kupata dhamana, ndipo waitishe kikao maalumu atakachoshiriki pia kamishna wa madini nchini.

Madiwani 10 akiwamo Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma wanashikiliwa na polisi wakiwemo wananchi watano na Katibu wa Vijana wa CCM wa Wilaya ya Geita, Ally Rajabu.

Kushikiliwa kwao kunatokana na vurugu zilizotokea Alhamisi iliyopita kwa madiwani kudaiwa kufunga barabara zinazoingia GGM wakishinikiza kulipwa Dola 12 milioni za Marekani (zaidi ya Sh26 bilioni zinazotokana na ushuru wa huduma kuanzia mwaka 2004 hadi 2013.

Kamishna wa madini nchini, Benjamin Mchwampaka jana alisema baada ya kumalizika kikao kilichohudhuriwa na kamati za ulinzi na usalama za mkoa na wilaya na ofisi ya madini ya mkoa kuwa hawakuendelea na kikao kingine kutokana na madiwani kutohudhuria.

Mchwampaka alisema lengo la kufika Geita ni kutafuta muafaka baina ya pande hizo lakini imeshindikana kutokana na baadhi ya madiwani kushikiliwa na vyombo vya dola na wengine kutohudhuria kikao hicho.

Madiwani hao wanasema fedha wanazoidai GGM ni haki yao kwa mujibu wa sheria kwa kuwa mgodi ulipaswa kulipa ushuru wa huduma wa asilimia 0.3 lakini hawakulipa na badala yake walilipa Dola 200,000 kwa mwaka tangu 2004 hadi 2013 kinyume cha sheria.

Hata hivyo, Meneja Uhusiano wa Jamii wa GGM, Manase Ndoroma alisema kinachosababisha mgogoro kati ya pande hizo ni kupingana kwa sheria ambazo zote zimetungwa na Bunge.

Alisema sheria ya madini iliwaruhusu kulipa Dola 200,000 kwa mwaka, huku sheria ya baraza la madiwani ikiwa imepitisha malipo ya asilimia 0.3 jambo linalosababisha mgogoro na suluhisho pekee ni kwenda mahakamani.

LIMETOLEWA AGIZO LA KUKAMATWA WAUAJI

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Agrey Mwanri ameviagiza vyombo vya Ulinzi na Usalama Mkoani humo kuwasaka watu wote waliohusika katika jaribio la mauaji ya watu wanne ambao walipigwa na kuwachoma moto katika kijiji cha Mwanabondo, Wilayani Uyui Mkoani humo kwa tuhuma za ushirikina.

Mwanri amesema kuwa vitendo vya wananchi kuendelea kujichukulia sheria mikono havivumiliki na havikubaliki hata kidogo kwa kuwa vyombo vya sheria vipo ambavyo vinaweza kutekeleza majukumu yake.

Mkuu huyo wa Mkoa ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa amesema licha ya tukio hilo kutokea lakini sio la kwanza hivyo vyombo vya usalama lazima vihakikishe vinawatia nguvuni watu wanaotekeleza matukio hayo.

Wakiongea wakiwa Hospitali Mkoani humo baadhi ya wahanga wa Tukio hilo wamesimulia jinsi walivyotaka kuuawa na watu hao wasiojulikana ambao walitokomea mara baada ya kushindwa kutekeleza azma yao.

KUTANA NA KIJANA WA MIAKA 17 ALIYETENGENEZA SIMU

Mo Omer anatarajia kuuza zaidi simu alizotengeneza katika mataifa hasa ya Afrika

Kijana wa miaka 17 kutoka nchini Canada ambaye alijitengenezea mwenyewe simu baada ya mama yake mSomali kusema kuwa hana uwezo wa kumnunulia simu ya smartphone amezungumza na BBC.

Mo Omer - ambaye anajiita mwenyewe "tech nerd" - alitengeneza simu ya smartphone kuanzia mwanzo , na anasema ataiuza kwa dola $180.

"Ina kila kitu unachoweza kukipata katika simu ya kawaida, ni kwamba tu haina gharama kubwa ," ameiambia BBC.

Simu "sio vifaa vigumu kutengeneza", aliongeza- na akasema ana azma ya kuzipeleka katika baadhi ya maeneo ya Afrika.

"Tumepokea maombi kutoka Nigeria na Algeria na maeneo mengine mengi. Ni soko linalokua kwa kasi ambalo tungependa kuingia ".

BBC

KILICHOFANYA UTETEZI WA MANJI KUSOGEZWA HADI SEPT 25

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, 'imepiga kalenda' kusikiliza ushahidi wa utetezi wa kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya heroin inayomkabili mfanyabiashara Yusufally Manji.

Kesi hiyo 'imepigwa kalenda' baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Timon Vitalis kuwa na udhuru wa kikazi na Hakimu Mkazi Mkuu, Mfawidhi, Cyprian Mkeha anayeisikiliza kuridhia ombi la Jamhuri.

Vitalis alidai jana kesi hiyo, ilipangwa kuendelea na ushahidi wa utetezi, lakini amepata udhuru wa kikazi na kuomba tarehe nyingine ya kuendelea.

Hakimu alisema kesi hiyo itasikilizwa mfululizo kuanzia Jumatatu mpaka Jumatano ijayo.

Kabla ya kupangwa tarehe nyingine ya kusikiliza kesi hiyo, hakimu alimuonya Manji kwa kuchelewa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake.

Manji alidai kuwa aliwasiliana na wakili wake kwasababu alikwenda hospitali na kwamba tukio hilo halitajirudia tena.

Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa kati ya Februari 6 na 9, mwaka huu eneo la Upanga Sea View, jijini Dar es Salaam, Manji alitumia dawa za kulevya aina ya heroin.

UCHAGUZI KENYA KUAHIRISHWA

UCHAGUZI wa marudio wa urais nchini Kenya huenda ukaahirishwa kutoka tarehe 17 mwezi ujao.

Tume ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC, imekuwa ikikutana kuangalia uwezekano wa kuahirisha Uchaguzi huu baada ya kampuni ya Ufaransa ya Safran Morpho kuomba muda zaidi kuboresha mitambo inayotumiwa kuwatambua wapiga kura.

Mbali na hilo, Muungano wa Upinzani Nasa, unaoongozwa na Raila Odinga, umesema Uchaguzi hautafanyika iwapo marekebisho hayatafanyika ndani ya Tume ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kujiuzulu kwa Ezra Chiloba Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo.

Chama cha Jubilee cha rais Uhuru Kenyatta kinashutumu shinikizo hilo la upinzani na kusisitiza uchaguzi ufanyike kama ulivyopangwa.

Saturday, September 9, 2017

JINSI UNAVYOWEZA KUWA SUMAKU YA FEDHA, NJIA 10 ZA KUIVUTA FEDHA IJE KWAKO MUDA WOTE

Linapokuja swala la fedha, kila mtu ana hisia tofauti, na hisia hizi zinatokana na malezi ambayo tumepata kwenye jamii ambazo tumekulia. Na katika hisia hizi, nyingi huwa ni hasi, kwamba fedha ni kitu kibaya au kitu ambacho hakihitaji kujadiliwa mara kwa mara. 

Kwa kusoma tu hiko kichwa cha habari kwamba kuna namna unaweza kuwa sumaku ya fedha, kuna watu tayari wameshakuwa hasi, kwamba kwa nini huyu Makirita anaandika kuhusu fedha, kwanza yeye anazo kiasi gani, na mengine mengi. Nakuelewa kama wewe ni mmoja wa watu wenye hisia hizi hasi, kwa sababu halikuwa kosa lako kuwa nazo, ila kama utasoma hapa mpaka mwisho na ukaendelea kuwa na hisia hizo, hapo sasa ni kosa lako. 

Tutakachokwenda kujifunza hapa ni kwamba wewe unaweza kuivuta fedha ije kwako, na kwa njia za kawaida kabisa, wala sio kwa nguvu ambazo hazieleweki kama wengi wanavyodanganyana. Zipo njia zilizodhibitishwa kisayansi ambazo zinafanya kazi kwa watu wote bila ya kujali kiwango cha elimu, rangi, au unatokea familia gani. 

Nina hakika umewahi kusikia usemi kwamba mwenye nacho huongezewa, ya kwamba tajiri ataendelea kuwa tajiri na masikini ataendelea kuwa masikini. Huu ni usemi uliowekwa na watu walioliona hilo likiendelea kwa wengi, lakini wakashindwa kulichimba kwa undani. Ukweli ni kwamba tajiri anaendelea kuwa tajiri kwa sababu ameshakuwa sumaku ya fedha, anajua jinsi ya kuzivuta zije kwake. Na masikini anaendelea kuwa masikini kwa sababu hajaijua mbinu ya kuzivuta fedha zije kwake. Je unataka kuzijua mbinu za kuvutia fedha zije kwako? 

Karibu tujifunze mambo haya kumi unayoweza kuanza kufanya leo kwenye maisha yako na ukazivutia fedha kuja kwako. 

1. Kuwa mkarimu, wasaidie wengine kwa chochote unachofanya. 
Njia ya kwanza kabisa ya kuzivutia fedha kuja kwako ni kuwa mkarimu. Chochote kile ambacho unakifanya kwenye maisha yako, iwe kazi au biashara, hakikisha lengo la kwanza ni kuwasaidia watu. Unawasaidia watu kwa kuwapa huduma ambazo ni bora na zinawaondolea maumivu wanayopata sasa au kuwapatia mahitaji wanayokosa sasa. 

2. Kuwa na shukrani kwa fedha ulizonazo. 
Haijalishi ni fedha kiasi gani unapata, hata kama ni kidogo sana, kitu muhimu kabisa ni kushukuru. Shukuru kwamba umepata nafasi ya kupata kiasi hiko cha fedha, ukijua ya kwamba kuna wengine wengi ambao hawajapata nafasi kama yako. Ukikutana na shilingi mia njiani wakati unapita, iokote kwa furaha. 

Unapokuwa mtu wa shukrani unakaribisha zaidi kile ambacho unashukuru. Wengi huwa walalamikaji kwa fedha kidogo wanazopata na hapa wanafukuza zaidi nafasi yoyote ya kupata zaidi. Kuwa mtu wa shukrani, utavutia fedha nyingi zaidi. 

3. Usiwaonee wivu wengine. 
Kama kuna watu wengine wenye fedha nyingi kuliko wewe, usiwaonee wivu, badala yake wabariki. Mafanikio ya wengine siyo sababu ya wewe kushindwa. Na unapojenga wivu dhidi ya wengine unaiambia akili yako kwamba kuwa na fedha siyo kitu kizuri na hivyo inazikimbia fursa za fedha. Lakini unapowabariki wale wenye fedha kuliko wewe, unaifungua akili yako na kuziona fursa nyingi zaidi za kifedha. 

4. Usijione mwenye hatia kwa kuwa una fedha nyingi. 
Moja ya vitu vinavyowafanya wengi kutokuvutia fedha ni kujiona kama wakiwa na fedha nyingi basi wale wanaowazunguka hawatajisikia vizuri. Huku ni kujiona mwenye hatia kama utakuwa na fedha. Na kujiona mwenye hatia kutaiambia akili yako iepuke mazingira yoyote yanayoweza kukuletea fedha zaidi. Jione kuwa wa msaada kama utakuwa na fedha nyingi zaidi, na utazivutia zaidi na zaidi. 

5. Kuwa na mapenzi makubwa kwenye kile unachofanya. 
Chochote unachofanya kwenye maisha yako, jambo muhimu kabisa ni ukipende sana. Penda kile unachofanya. Kuna usemi unasema kama kazi yako ni kitu unachopenda, hutafanya kazi kwenye maisha yako. Na mwingine fanya kile unachopenda na fedha haitakuwa tatizo kwako. Fanya kitu unachopenda kufanya, iwe ni kazi au biashara, na weka moyo wako wote kwenye kitu hiko na hakuna kitu kinaweza kukuzuia wewe kupata fedha zaidi. 
Wengi wamekuwa wakifanya vitu ambavyo hawavipendi ili tu wapate fedha, na wanashangaa kwa nini hawazipati, jibu ni kwa sababu wanazifukuza wao wenyewe. Unapofanya unachopenda, unazivutia fedha kuja kwako. 

6. Ukipoteza fedha, usijione mnyonge na kulalamika. 
Pale unapopoteza fedha, na lazima utapoteza iwe ni kwa hasara au kudhulumiwa, usianze kulalamika kwa nini inatokea kwako tu, bali jifunze ni nini kimepelekea wewe kufikia kwenye hali hiyo. Na hakikisha hurudii tena makosa ambayo uliyafanya awali na yakakufikisha hapo. Labda unahitaji kuwa makini zaidi, labda unahitaji kuangalia wale unaowaamini na mengine mengi. 
Ukiishia tu kulalamika na kuona wewe huna hatia, utaendelea kurudia makosa yale yale na kamwe hutazivutia fedha kuja kwako. 

7. Siku zote timiza ahadi zako. 
Fanya kile ambacho umeahidi utafanya, na kikamilishe kwa wakati na kwa ubora. Usiwe mtu wa kuahidi kwa maneno na wakati wa matendo huonekani. Timiza ahadi zako na utavutia fedha nyingi zaidi kwako. Iwe ni kwenye kazi au kwenye biashara, unachomwahidi mwajiri wako kitimize, na hatakuwa na jinsi bali kukuthamini zaidi. Chochote unachomwahidi mteja wako timiza, na atapata huduma bora zitakazomfanya awe mteja wako wa kudumu na kuwaambia wengine wengi zaidi. 

8. Tegemea kuwa tajiri. 
Haijalishi maana yako ya utajiri ni nini, tegemea kuwa tajiri. Na usiishie tu kutegemea bali kuwa na mpango kabisa wa jinsi gani utafikia utajiri wako, kipato chako kiwe kiasi gani, uwekeze kiasi gani ili uweze kufikia utajiri. Utajiri hauji kama ajali, ni zao la malengo, mipango na juhudi kubwa. Kama hutegemei kuwa tajiri huwezi kuvutia fedha kwako. 

9. Amini kwenye wingi. 
Kuna fedha nyingi sana kwenye dunia hii, nyingi mno, japo wengi wanakushawishi kwamba kuna uhaba wa fedha, siyo kweli. Amini kwenye wingi wa fedha na unachohitaji ni wewe kuja na wazo zuri la kuwasaidia watu na watakuwa tayari kukupa fedha zaidi na zaidi. Dunia haina uhaba wa fedha na mali, bali ina uhaba wa mawazo mazuri ya kuboresha maisha, njoo na mawazo mazuri na utavutia fedha zaidi na zaidi. 

10. Kuwa mkweli kwako, kuwa halisi. 
Linapokuja swala la fedha na utajiri, watu wengi sana sio wa kweli kwao binafsi na hata kwa wengine. Watu wengi sio halisi, bali ni feki, wengi wanaigiza maisha ya utajiri na wakati hali zao sivyo zilivyo. Wengi wanakazana waonekane kwa nje wana utajiri kumbe ndani yao mambo ni magumu. Watu wanaingia kwenye madeni makubwa ili tu kuonekana nao wapo. Hii sio njia nzuri ya kuvutia fedha zije kwako, badala yake utazikimbiza zaidi. Njia bora ya kuvutia fedha kuja kwako ni kuwa mkweli, na kuwa halisi. Ishi yale maisha ambayo ni yako, usitake kuleta maigizo, hakuna yeyote unayemfaidisha na badala yake unajiumiza mwenyewe. 

Hizo ndiyo njia kumi za kuzivutia fedha zije kwako na hatimaye uwe tajiri. Wote tunajua fedha ni muhimu, na kadiri unavyokuwa nazo nyingi inakuwa rahisi kwako kupata mahitaji ya msingi ya maisha yako, na hata kuwasaidia wengine pia. 

Njia zote hizi kumi zinaanza na wewe binafsi, haiangalii elimu yako ni kiasi gani, rangi ya ngozi yako, au kabila unalotokea. Pia haziangalii umri wako au umetoka familia ya aina gani. Ni wewe ufanye maamuzi leo na uanze kutekeleza hayo. Na ujue inachukua muda, siyo jambo la kutokea mara moja, hivyo kuwa mvumulivu. 

Neno la mwisho kabisa ninalotaka kukushirikisha ni kukuambia uchukue hatua, iwe utayafanyia haya kazi, au utayakataa na kuendelea na maisha yako ya sasa. Maamuzi ni yako wewe mwenyewe. Lakini jua hakuna mtu atakayekuja kukutoa hapo ulipo, utajitoa wewe mwenyewe. 

Tuesday, August 8, 2017

NIYONZIMA : TUKUTANE UWANJANI



KIUNGO Mshambuliaji wa Simba raia wa Rwanda, Haruna Niyonzima ametambulishwa rasmi katika kikosi cha timu hiyo na anatarajiwa kuwa mmoja wa wachezaji watakaoshuka dimbani leo Jumanne katika mchezo wa Simba Day dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda kwenye Uwanja wa Taifa, Dar. 

Niyonzima aliyejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Yanga, jana Jumatatu asubuhi alifanya mazoezi kwa mara ya kwanza na timu yake hiyo mpya kabla ya kutambulishwa mchana mbele ya waandishi wa habari kwenye makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo Kariakoo jijini Dar. 

Akizungumza mara baada ya kutambulishwa, Niyonzima alisema yeye kwa sasa ni mchezaji wa Simba hivyo mashabiki wasubirie kuona kazi yake uwanjani. “Mimi kwa sasa ni mchezaji wa Simba, mambo mengine yataonekana uwanjani, sina cha ziada cha kuzungumza,” alisema Niyonzima. 

Niyonzima (kushoto) akifanya mazoezi kwa kufuata maelekezo ya kocha msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja. 
Aidha, Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja, alisema: “Tuna timu nzuri yenye wachezaji wazuri na uongozi umeweza kutupeleka kambi Afrika Kusini na tumeweza kucheza mechi mbili za kirafiki, tumeona viwango vya wachezaji wetu na mechi ya kesho ‘leo’ itatusaidia kuangalia fitnes za wachezaji wetu, na tumejiandaa vizuri kwa ajili ya ligi.” 

Naye, nahodha wa Simba, Method Mwanjale alisema msimu huu watakuwa na kikosi kizuri ambacho kitawasaidia kuleta ushindani katika ligi na michuano mbalimbali. Aidha, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara aliyekuwa akiwatambulisha wachezaji hao, alisema Rayon Sports ilitarajiwa kuwasili nchini jana saa 3:00 usiku kwa ajili ya mechi hiyo ambayo itatanguliwa na mechi ya Simba B dhidi ya Rangers. 

Mgeni rasmi katika Tamasha la Simba Day anatarajiwa kuwa Januari Makamba ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Anayeshughulikia Muungano na Mazingira na kudai kuwa uwanja utafunguliwa kuanzia saa 4:00 asubuhi. 

Manara aliongeza kuwa leo itakuwa siku maalumu ya kumkabidhi Tuzo ya Mchezaji Bora ya Mashabiki beki wake, Mohammed Hussein ‘Zimbwe Jr’.

Tuesday, July 25, 2017

JPM' AMTOLEA UVIVU LISSU





Rais John Magufuli amesema kuwa Serikali imetatua Changamoto mbalimbali pamoja na Madawati  kwenye Jimbo la Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu. 

"Tumetatua changamoto ya madawati...sasa hivi hata watoto wa TunduLissu wanakaa" 

Magufuli amesema kuwa kuna "Wengine mmewachagua lakini wanaongelea ya Dar es Salaam tu...Kosea kuoa unaweza kutoa talaka, lakini usikosee kuchagua"

Sunday, July 23, 2017

MISINGI BORA YA KUFUATA ILI KUJENGA AFYA YA MWILI WAKO



Katika maisha moja ya kitu cha msingi sana ambacho hutakiwi kukikosa ni afya bora. Kosa yote, lakini usikose afya bora, afya bora ina muunganiko na mambo mengi sana kwenye maisha yako ikiwa pamoja na mafanikio. 

Naomba uelewe hivi, unapokuwa hauna afya nzuri, hakuna ambacho unaweza ukakifanikisha, utashindwa kwenye mambo mengi kwa sababu ya kushindwa kuweza kuyafanya kwa ufanisi kutokana na tatizo la afya yako. 

Kwa mantiki hiyo,  mpaka hapo unaona ni kwa namna gani afya ilivyokuwa ya muhimu sana kwenye maisha yako. Sio suala la kuhoji tena ni lazima uwe na afya bora. Ni kwa namna gani utaweza kutengeneza afya bora? 

Ifuatayo Ni Misingi Bora Ya Kufuata Ili Kujenga Afya Ya Mwili Wako. 

Msingi wa kwanza,  kunywa maji kwa wingi. 
Maji mengi mwili yanasaidia mwili wako kuwa katika hali nzuri wakati wote na kusababisha baadhi ya viungo kufanya kazi kwa ufasaha. Hivyo, unalazimika kunywa maji kwa wingi kila wakati ili kuweza kulinda afya ya mwili wako ili iwe bora wakati wote, kinyume cha hapo itakuwa ni shida kwako. 

Msingi wa pili, soma kabla hujalala. 
Unaposoma kitu kipya kabala hujalala unaifanya akili yake iende kupumzika huku ikiwa na wazo jipya au kitu cha kufanyia kazi usiku wote. Ukumbuke hapa mawazo yako ya kina yanafanya kazi muda wote kwa saa 24 . Soma kitu kipya chanya angalau nusu saa kabla hujalala kila siku itakusaidia sana. 

Msingi wa tatu, fanya tahajudi (Meditation). 
Tafuta eneo lilotulia na kila siku jitahidi kufanya tahajudi ama ‘meditation.’ Hiki ni kipindi ambacho unatakiwa ukae kwa utulivu ukitafakari maisha yako na kutafakari kile unachokitaka katika maisha. Unaweza ukafanya tahajudi/meditation angalau hata kwa dakika 15 kila siku.

Msingi wanne,  fanya mazoezi. 
Unatakiwa pia ujenge tabia ya kufanya mazoezi kila siku ili kuupa mwili wako afya. Fanya mazoezi ya kukimbia, fanya mazoezi ya kuruka au fanya mazoezi ya kunyanyua vitu vizito. Ukifanya mazoezi kila siku na ikawa ndio kitu endelevu mwili wako utakaa katika afya nzuri sana kila wakati. 

Msingi wa tano, kula chakula bora. 
Mwili wako haujengwi kwa matofali, mwili wako unajengwa kwa chakula safi. Kwa kulijua hili kila wakati jitahidi sana kuulisha mwili wako chakula ambacho kitakusaidia wewe kuweza kuujenga mwili wako kwa  afya bora. Tafuta vyakula safi vitakavyo ulinda mwili wako na magonjwa. 

Kimsingi, afya yako haijengwi kwa kubahatisha. Afya inajengwa kwa kuzingatia msingi ya afya bora kama ilivyoainishwa katika makala haya ya leo. Usisubiri hadi uende kwa daktari, zingatia mambo haya nawe utakuwa na afya bora.

KISA CHA JUSTIN BIEBER KUPIGWA MARUFUKU CHINA


Nyota wa muziki wa Pop kutoka Canada Justin Bieber amepigwa marufuku kutumbuiza nchini China, kwa mujibu wa Wizara ya Utamaduni nchini humo.

Taarifa ya wizara hiyo imesema haifai kwa watumbuizaji ambao wamejihusisha katika "utovu wa nidhamu" kuruhusiwa kuingia nchini humo.

"Justin Bieber ni mwimbaji mwenye kipaji, lakini pia ni mwanamuziki kijana mwenye kuzua utata," amesema.

Taarifa hiyo imetolewa kujibu swali lililokuwa limeulizwa na mmoja wa watu katika tovuti ya wizara hiyo.

"Twatumai kwamba Justin Bieber atakapokomaa, anaweza kuendelea kuimarisha maneno yake na matendo, na kuwa mwanamuziki anayependwa kwa dhati na umma," taarifa hiyo imesema

Bieber aliwahi kuzuru China mwaka 2013, lakini sasa amejiunga na orodha ndefu ya wanamuziki waliopigwa marufuku nchini humo.

Wengine ni bendi ya Uingereza kwa jina Oasis na kundi la Marekani kwa jina Maroon 5, ambao wamepigwa marufuku kwa sababu ya misimamo yao ya kisiasa badala ya tabia.

Mwaka 2014, Bieber, maarufu kwa wimbo wake Sorry alizua utata baada ya kupakia picha aliyopigwa akitembelea madhabahu ya Yasukuni jijini Tokyo.

Madhabahu hayo nchini Japan yalijengwa kwa heshima ya wanajeshi waliouawa vitani pamoja na wahalifu wa kivita lakini nchini China na Korea Kusini, hutazamwa kama ishara kwamba Japan haijajutia makosa yaliyotendwa na watawala wa nchi hiyo China na Japan miaka ya nyuma.

Friday, March 31, 2017

BAADA YA RAIS ZUMA KUMTIMUA WAZIRI WA FEDHA, RAND YA AFRIKA KUSINI YASHUKA KWA KASI

Baada ya Rais Zuma kumtimua waziri wa fedha, rand ya Afrika Kusini yashuka kwa kasi

Fedha ya Afrika Kusini, rand, inaendelea kushuka thamani kwa kasi baada ya Rais Jacob Zuma kumtimua waziri wa fedha mwenye uzoefu mkubwa, Pravin Gordhan.

Zuma alitangaza uamuzi huo Alhamis hii kuwa anamuondoa Gordhan pamoja na mawaziri wengine. Wawekezaji walikuwa wameshaanza kuhofia kuwa Zuma angemtimua waziri huyo baada ya Jumatatu kumuamuru asitishe mikutano mingi na wawekezaji wa nje na kurudi nyumbani.

Hatua hiyo pia ilikuwa dhoruba kwa rand ambayo sasa imeshuka thamani yake kwa asilimia 8. Wachambuzi walionya mapema wiki hii kuwa kumuondoa Gordhan na mawaziri wengine kungekuwa na madhara.

Amekuwa waziri wa fedha kwa kipindi kirefu kuanzia mwaka 2009 hadi 2014 na kurudi tena December 2015. Zuma amteua Malusi Gigaba aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani kushika nafasi hiyo.

DO SLAA: MVUMILIENI MAGUFULI

Dk Slaa: Mvumilieni Magufuli

BAADA ya kuishi nchini Canada kwa zaidi miaka miwili sasa, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa amesema anakuna kichwa ili kupima mazingira yaliyomfanya aondoke nchini na familia yake kama yapo au laa.

Septemba,2015 wakati wa Uchaguzi Mkuu Dk. Slaa alijiweka kando na siasa, kwa kile alichokieleza kutofautiana na chama chake juu ya masharti ya kumpokea aliyekuwa mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),Edward Lowassa.

Hata hivyo Dk. Slaa ambaye amekuwa mbunge wa Karatu kwa vipindi vitatu mfululizo, hakuweza kuainisha mazingira yaliyomfanya aondokea nchini na kwenda kuishi ughaibuni.

“Sina tabia ya kuyumbishwa…sina chuki na mtu yeyote, sipendi siasa za udanganyifu na propaganda. Nimeachana na siasa tangu Julai 28,2015, baada ya kuona misingi ya chama nilichoshiriki kukijenga imepotoshwa,”alisema Dk. Slaa siku alipotangaza kuachana na siasa.

Pamoja na mambo mengine, alisema sharti la kwanza ambalo alitaka Chadema izingatie ni kiongozi huyo wa zamani ndani ya serikali ya CCM, kujisafisha dhidi ya tuhuma ya kashfa ya sakata la Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond aliyohusishwa nayo akiwa Waziri Mkuu.

Kurudi nchini

Akizungumza na MTANZANIA akiwa nchini Canada jana, Dk. Slaa alisema amemaliza masomo yake na baada ya kufanya tafakari atarejea nchini wakati wowote.

“Ni kweli nimemaliza masomo yangu. Bado napima mazingira yaliyonifanya niondoke na familia yangu. Baada ya hapo tutaangalia uwezekano wa kurejea,”alisema.

Alisema kuhusu matarajio yake ya kisiasa, watu wameshindwa kumwelewa siku ambayo alitangaza kustaafu siasa za vyama.

Alisema alichomaanisha ni kwamba, pamoja na kuachana na siasa za vyama,atakuwa tayari kupiga kelele pale anapoona masilahi ya Taifa yanaumia.

“Hadi sasa sijapiga kelele kwa kuwa sijaona masilahi ya Taifa yakiangamizwa, hatua mbalimbali zinazochukuliwa ni kweli zinawaumiza wasiohusika.

“Ndio maana nilitumia katika makala mojawapo mtego wa panya huwakamata wanaohusika na wasiohusika. Hivyo, makosa madogo mimi hayanisumbui kwa kuwa hakuna binadamu kamilifu ,”alisema.

Rais Magufuli

Akizungumzia utendaji wa Rais Dk. John Magufuli, alisema watu waelewe hakuna nchi hata moja ambapo kiongozi atakubalika na watu wote kwa asilimia 100.

Alisema wako watu ambao masilahi yao yataguswa kwa namna moja au nyingine hivyo lazima watapiga kelele.

Kutokana hilo, alisema Rais Dk. Magufuli katika kundi ambalo halihitaji fedha ameyatekeleza yote kwa asilimia 99.9, ikiwa ni pamoja na uwajibikaji serikalini, kuchukua hatua kali dhidi ya rushwa, uwizi wa mali za umma, uwindaji haramu na kudhibiti dawa za kulevya.

“Hatua zote zimechukuliwa,zinapaswa kuwa endelevu. Kwa bahati mbaya mchwa wengine waliopenya mpaka ndani ya Ikulu na Serikali na huwezi kufagia Serikali nzima kwa siku mmoja.

“Kwa jinsi Rais ambavyo hayumbi na wala hayumbishwi, nina hakika atafikia malengo na kurudisha Taifa kwenye misingi ya tunu za Taifa ya uwazi, ukweli, uadilifu, kuheshimiana na kuthaminiana na hasa kujali utu.

“Hii ndiyo hali ambayo JPM kila siku anaiita ‘Transition’ (kipindi cha mpito). Tutafika tu, tunatakiwa kuwa wavumilivu na wenye uzalendo wa kweli ana nia njema ya kufikisha Taifa mahali pazuri. Hii inahitaji kuweka pembeni maslahi yetu binafsi kama mtu mmoja mmoja, viongozi wa Serikali au hata wa kisiasa,”alisema Dk. Slaa.

Upinzani

Kuhusu mwenendo huo endapo utasaidia upinzani kuingia Ikulu 2020, Dk. Slaa alisema wakija na ajenda mbadala na makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja itawasaidia.

Dk. Slaa ambaye pia alipata kugombea urais kupitia Chadema mwaka 2010, alisema endapo wataendelea kurukia kauli za Rais, basi upinzani utafutika kabla ya 2020. 

“Kama nilivyorejea mara kadhaa, upinzani makini utaingia Ikulu kwa ajenda mbadala. Ajenda makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja katika kuwatoa kwenye kero zao mbalimbali.

“Hadi sasa ninachoona ni ‘kurukia’ kauli za JPM, lakini kauli si ajenda na hatupeani maksi kwa kuzungumzia usahihi wa lugha. Wako wanaotazama usahihi wa lugha na mahali pa kutazama usahihi huo. Kimsingi hayo ni masuala ya darasani au kwenye uandishi wa vitabu.

“Aidha kumtuhumu JPM kukiuka Katiba na sheria nayo haina tija. Wote wanaomtuhumu wanajua kuwa wakiambiwa waonyeshe kifungu mahususi alichokiuka yeye mwenyewe katika utendaji wake hawana majibu ya kuridhisha.

“Hivyo mimi sijaona mwenendo wa JPM unaosaidia kuingiza upinzani Ikulu. Isitoshe kama hawatakuja na ajenda makini na mkakati ulioandaliwa unaowatoa wananchi hapa walipo kwenda kwenye raha, upinzani unaweza kufutika kabla ya 2020,”alisema Dk. Slaa.

Thursday, March 30, 2017

MWAROBAINI KAZI YAKE KWENYE NGOZI

   Dk. Fadhili Emilly
Leo hii kupitia ukurasa wetu huu nimeona tufahamishane kuhusu faida za mti wa mwarobaini hasa katika suala zima la magonjwa ya ngozi yanayosumbua sana wanadamu.

  
   Mwarobaini (Azadirachta indica) ni mti unaofahamika kwa uwezo wake wa kutibu magonjwa ya aina mbalimbali. Inaaminika kuwa mti huu asili yake ni nchini India na Burma. Mwarobaini hushamiri zaidi katika nchi za tropiki na una uwezo mkubwa wa kuhimili ukame.

 
   Hapa nchini Tanzania, mti wa mwarobaini huweza kupatikana kwa urahisi kabisa katika maeneo mengi ya mijini na vijijini pia.
Jina hili la ‘mwarobaini’ linatokana na imani kuwa mti huu una uwezo wa kutibu magonjwa yapatayo arobaini, huku majani yake na mbegu zikitumiwa kama tiba kwa miaka mingi katika nchi mbalimbali duniani.

 
     Kati ya magonjwa ambayo mti huu umetumika kutibu au kupoza ni pamoja na matatizo ya kusaga chakula tumboni, kisukari, saratani, magonjwa ya ngozi, malaria, ukungu (fungus), n.k.
 
    
      Pia matawi ya mti huu hutumiwa kama mswaki na magome yake hutumiwa kama dawa ya kusafisha meno.
Hali kadhalika mafuta ya mbegu ya mwarobaini hutumika kutengenezea vipodozi na sabuni, lakini pia mbegu au mafuta yake hutumiwa kama dawa ya kuulia wadudu wanaoharibu mimea shambani.

    Baada ya kufahamu baadhi ya faida mbalimbali za mti wa mwarobaini, leo nitakufundisha namna ya kutumia mti wa mwarobaini kujitibu magonjwa ya ngozi.

   
Mahitaji
Majani ya mti wa mwarobaini.
Sufuria
Mwiko
Jiko la gesi, mkaa au jiko la mafuta.
Hatua za kufuata
1. Chukua majani mabichi ya mti wa mwarobaini na uyaweke kwenye sufuria.

2. Chukua sufuria yako yenye majani ya mti wa mwarobaini na uiinjike kwenye jiko lenye moto wa wastani.

3. Chukua mwiko wako na uanze kuyakoroga majani yako taratibu hadi yakauke bila kuungua.

4. Majani yako yakishakauka, ipua sufuria yako, chukua majani yako yaliyokauka, yasage kisha hifadhi unga unga wako kwenye chombo cha plastiki.

Matumizi
Tumia vijiko viwili vya chai kwenye kikombe cha robo lita chenye maji ya moto, fanya hivyo mara mbili kwa siku kwa muda wa siku ishirini na moja.

RIPOTI: TANZANIA IMETAJWA KUONGOZA AFRIKA KWENYE HILI

Ripoti: Tanzania imetajwa kuongoza Afrika kwenye hili...


Tanzania imechangia asilimia 19.3 ya jumla ya wageni wa kimataifa kupitia anga (international air arrivals) ukilinganisha na asilimia 18.2 ya Kenya, asilimia 17.2 Misri na asilimia 12.1 ya Afrika Kusini katika kipindi cha kuanzia September 2016 hadi January 2017.


Takwimu hizi ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la ufuatiliaji wa masuala usafiri wa ndege, ForwardKeys ambayo hulinganisha ukataji tiketi za ndege zaidi ya milioni 16 kila siku ili kuiweka Afrika kwenye ramani ya utalii duniani.

Kwa jumla, Afrika Mashariki ina asimilia 16.4 ya ufikaji wa wageni kwa njia ya anga. Na kwa ujumla pia, kuna ongezeko la asilimia 10.3 ya ufikaji wageni Afrika. Soma zaidi ripoti hiyo hapa.

Sunday, March 26, 2017

KUPUNGUZA KIWANGO CHA CHUMVI HUZUIA KWENDA CHOONI USIKU

Watu ambao huamka usiku kwa minajili ya kuenda chooni, wanahitaji kupunguza kiwango cha chumvi katika chakula chao, kwa mujibu wa madaktari nchini Japan.

Tatizo hilo linalofahamika kama nocturia, ambapo mara nyingi huwaathiri watu walio na zaidi ya miaka 60, husababisho matatizo ya kupata usingizi na linaweza kuathiri maisha ya mtu.

Uchunguzi huo uliofanyiwa zaidi ya watu 300 wa kujitolea, uligundua kuwa kupunguza kiwango cha chumvi kwenye chakula, humwezesha mtu kupunguza safari za kuenda haja ndogo.

Watafiti kutoka chuo cha Nagasaki , waliwasilisha matokeo yao kwenye warsha moja ya sayansi mjini London.

Walichunguza wagonjwa waliokuwa wakitumia kiwango kikubwa cha chumvi pamoja na matatizo ya kulala kwa miezi mitatu baada ya kuwapa ushauri wa kupunguza kiwangi hicho kwenyeychakula chao.

Safari za kuenda chooni zilipungua kwa zaidi ya mara mbili kila siku hadi safari moja.
Hiyo pia ilishuhudiwa mchana na maisha ya watu hao pia yakaimarika.

Hitaji la kuamka usiku kwa haja ndogo huwaathiri zaidi ya nusu ya wanaume na wanawake walio na zaidi ya miaka 50.

Hali hiyo ni kawaida kwa watu wazee ambao wengi wao huamka takrban mara mbili kwa usiku.
Mtu anapofanya safari nyindgi chooni usiku, hupata matatizo ya kulala, hali ambayo husababisha pia msongo na uchovu.

MBIO ZAMFANYA HARMORAPA KUPATA DILI NONO KWENYE KINYWAJI CHA SWALA

Mbio zamfanya Harmorapa kupata dili nono kwenye kinywaji cha Swala


MSANII wa Bongo Fleva anayetrendi katika mitandao ya kijamii Bongo, ‘Hamorapa’ anatazamiwa kuwa balozi wa Kinywaji kiitwacho Swala.

Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu, Hamorapa amefunguka kuwa yupo katika mazungumzo na kampuni inayozalisha kinywaji hicho na anatarajia kupata dili nono ya kukitangaza kinywaji hicho.

JWTZ YAILIPIA TANESCO BILLIONI 1 KATI YA BILLIONI 3 AMBAZO WANADAIWA NA SHIRIKA HILO LA UMEME

JWTZ yadaiwa na Tanesco Sh3bilioni

Dar es Salaam. Mkuu wa Majeshi nchini, Evance Mabeyo amesema Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) linadaiwa Sh3 bilioni na Shirika la Umeme nchini na kesho (Jumatatu)  watapunguza deni hilo ili wasikatiwe umeme.

Mabeyo ameyasema hayo leo wakati anazungumza na waandishi wa habari makao makuu ya jeshi (Ngome) na kueleza deni hilo limetokana na shughuli za jeshi hilo kwenye ulinzi wa Taifa pamoja na ufinyu wa bajeti.

"Baada ya kupokea maelezo ya Tanesco na kufuatia tamko la Rais, Jeshi la Wananchi limetafakari na limefanya jitihada kupata fedha za  kupunguza deni hili, tunadaiwa fedha kiasi kinachozi kidogo Sh3 bilioni, nimeagiza watendaji wetu watafute Sh1 bilioni," amesema Mabeyo.

Mabeyo amesema juhudi zinazofanywa na Jeshi hilo zinatakiwa kuonyeshwa na Taasisi nyingine ili kuweza kuiongezea Tanesco uwezo wa kutoa huduma.

ENEO AMBAPO WATOTO HUPEWA MAJINA YA KUSTAAJABISHA

Eneo ambapo watoto hupewa majina ya kustaajabisha

Katika eneo moja mashariki mwa Zambia mwandishi wa BBC Chris Haslam, anakumbana na kijana mdogo ambaye anajikakamua kusukuma baiskeli kubwa ambayo imebeba mitungi ya maji, kuni na mfuko wa mchele.

Kwa vile kijana anaisukuma baiskeli hiyo na mikono yake miwili, hana njia ya kuwafukuza nzi kutoka kwa macho yake.


Jina lake ni "Mulangani". Jina hilo ni la jamii ya Nguni linalomaanisha "niadhibu" au yule ambaye ni lazima adhibiwe. Chris Haslam alimuuliza dereva kuhusu ni nani anayeweza kumpa mtota wake jina baya kama hilo?

"Labda babu yake au chifu," dereva akajibu. Nchini Zambia na hata Zimbabwehasa mashambani , ni jambo la kawaida wazazi kuwaalika wazee wa jamii kuwapa majina watoto wanapozaliwa.

Mara nyingine chifu huwa anataka kuiadhibu familia, anasema dereva, "au anafikiri kuwa mtoto aliyezaliwa ni mzigo kwa familia."

Lakini kijana huyo si peke yake aliye na jina la kutisha. Baadaye anakutana na "Chilumba", jina linalomaansiha "kaburi la ndugu yangu"

Kisha anakutana na Balaudye - "nitaliwa" na Chakufwa- "amekufa"

Pia anakutana na Daliso linalomaanisha "baraka" na Chikondi linalomaanisa "upendo".

Kwenye utamaduni wa Afrika kuna tabia ya kuwapa watoto majina kutokana na nyakati walizozaliwa, kwa mujibu wa Clare Mulkenga afisa wa huduma za watoto nchini Zambia.

Anasema kuwa hata hivyo ni vyema kwa wale wanaozaliwa nyakati nzuri lakini pia huwa ni bahati mbaya kwa wengine.

MGOGORO MZITO UNARIPOTIWA NDANI YA CHADEMA

Mgogoro mzito unaripotiwa ndani ya CHADEMA


Chama chama Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kimeingia katika wingu zito na kutishia kukisambaratisha chama hicho.

Chanzo cha Mgogoro ni nafasi za Ubunge wa Africa mashariki, Uchaguzi wa kanda ya Mashariki na Hali ya kifedha ndani ya chama.

Chanzo cha ndani ya CHADEMA kinasema kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Ndugu Freeman Mbowe aliingia na majina mawili ndo akawaambia wayachague ambapo aliingia na Majina hayo ni Masha na Wenje hakukua na utaratibu sahihi wa kuwapata wagombea katika Bunge la Africa Mashariki.

Uchaguzi wa kumpata Viongozi ndani ya kanda ya Mashariki ulijaa kasoro nyingi ambapo wananchama wanaulinganisha na ule wa kanda ya Nyasa ambapo Ole Sosopi alitupwa nje ya kinyang'anyiro kwa kuwa mwenyekiti wa chama aliingia na Jina lake.

Idara ya fedha ndani ya CHADEMA haijakaa vizuri hivyo kuleta sintofahamu kwa wadhamini ambao wanataka ukaguzi wa fedha kupitia mkaguzi huru akague ili wajiridhishe wadhamini ndani ya CHADEMA wamekua wagumu kutoa fedha zao Hali ambayo inaisababishia chama ukata kwani Tajiri na Mdhamini mkubwa ndani ya CHADEMA ndugu Sabodo Alishajitoa na Kuungana na Rais Magufuli baada ya kuona Utendaji wake uliotukuka.

BASATA WAMEZUNGUMZIA WIMBO WA NAY WA MITEGO

BASATA Wamezungumzia Wimbo wa Nay Wa Mitego

Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Godfrey Mngereza amesema wataufungia wimbo wa 'Wapo' wa Nay wa Mitego kwani hauna maadili.


ASICHOTAKA KUKISIKIA KABISA KWENYE SOKA WAZIRI MWAKYEMBE

Asichotaka kukisikia kabisa kwenye Soka Waziri Mwakyembe


Waziri wa Mpya wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ameanza kazi katika Wizara mpya. 

Lakini Dk Mwakyembe ambaye kitaalamu ni mwandishi wa habari na mwanasheria nguli, amesema hapendi kuona timu za Tanzania zinafungwafungwa tu.

 "Watanzania tumechoka na huu uteja, kusukumwa sukumwa tu kwenye soka. Ni hamu ya watanzania sasa tuonekane katika ulimwengu wa soka", amesema Waziri Dk. Mwakyembe aliyezungumza na Kamati ya Hamasa kwa Serengeti Boys alipokutana nayo kwa mara ya kwanza jana Machi 25, mwaka huu.

Waziri alikwenda mbali kwa kuiagiza Wizara yake yote ijikite kuhakikisha maandalizi ya Serengeti Boys yanakamilika kwa wakati. 

"Nataka Wizara yangu yote sasa wimbo wetu uwe Serengeti Boys," amesema Dk. Mwakyembe.

Katika hafla hiyo, Dk Mwakyembe amempongeza mtangulizi wake, Mheshimiwa Nape Nnauye kwa kuunda Kamati ya Serengeti Boys ili kutoa hamasa ya Watanzania kwa timu yao. 

Alisema Serengeti Boys ni nyota wanaoinukia (upcoming stars) na wanampa sababu ya kuanza kwenda mpirani tena. 

Waziri Dk Mwakyembe aliendelea kusema kuwa michezo ya leo inahitaji uwekezaji hivyo Wizara yake itahakikisha kuwa jukumu hilo analibeba.

"Naona kama imechelewa, lakini bado muda upo, tukimbie, nataka Wizara nzima wimbo wetu uwe Serengeti Boys", alisema kwa hamasa kubwa. 

Dk Mwakyembe amempongeza Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Mwenyekiti wa Kamati ya Serengeti Boys, Charles Hilary kwa mafanikio ya program ya mageuzi ya soka nchini. 

Naye Mkurugenzi wa Michezo katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Yussuf Singo alisema sasa imechoka kuwa kichwa cha mwenda wazimu na hivyo Taifa limeazimia kucheza Kombe la Dunia kupitia vijana wa Serengeti Boys. 

Rais wa Shirikisho la Kandanda Tanzania, Jamal Malinzi alisema kufuzu kwa Serengeti Boys kucheza fainali za AFCON ni sifa pekee na mwanzo mpya wa mageuzi makubwa ya soka la Tanzania.

Amesema maandalizi ya ushiriki wa fainali za AFCON zitahitaji takriban Shilingi bilioni moja. 

Amesema mikakati mbalimbali imeandaliwa kuchangisha kiasi hicho cha fedha, ikiwa ni pamoja na kuandaa chakula cha hisani. 

Waziri Mwakyembe amesema atahakikisha fedha hiyo inapatikana ili vijana wa Serengeti Boys waweze kufuzu kucheza kombe la dunia huko India mwishoni mwa mwaka huu.

NAY WA MITEGO ALIVYKKUWA NDANI YA KITUO CHA POLISI MOROGORO

PICHA: Nay Wa Mitego alivyokuwa ndani ya kituo cha polisi Morogoro

Hapo chini ni Picha ikimuonesha Nay wa Mitego akiwa ndani ya kituo cha Polisi Morogoro baada ya kukamatwa. (Picha kwa hisani ya Group la WhatsApp la Waandishi wa Morogoro)





HAYA NDIYO MAAJABU MENGINE YA MTI WA MWAROBAINI

Haya ndiyo majabu mengine ya mti wa mwarobaini

Mwarobaini ni mti maarufu sana na unajulikana karibu kila mahali , licha ya kujulikana kila mahali mti huu una kivuli mwanana. Lakini jina hili la mti huo limetokana na uwezo wake wa kutibu zaidi ya magonjwa arobaini. Ingawaje mti huu si majani wala mizizi ni mchungu mno kwa mtumiaji.

Lakini inasadikia kuwa mti huu asili yake imetokea nchini ondoa,  na pia ina uwezo mkubwa wa kustawi sehemu zenye ukame zaidi.  Kwa hapa Tanzania ukienda maeneo ya Dodoma utakubaliana na ukweli huu.

Labda tuangazie macho japo kwa uchache kwa kuona maajabu ya mti huu kama ifuatavyo.

1. Mwarobaini ni dawa ya kuua minyoo yote tumboni,

2. Hutubu homa, hasa zile homa za usiku

3. Mwarobaini hutibu kikohozi.

4. Mwili kuwaka moto.

5.kuharisha pamoja na tatizo la vidonda vya tumbo. Chukua majani ya mmea huu kisha yatafune bila kujali uchungu yaliyo nayo.

6.Mwarobaini hutubu matatizo ya macho.

Ili kutibu matatizo ya macho Unachotakiwa kufanya ni kufuata maelekezo kama amabayo nitaeleza hapo chini.

7.magonjwa mbalimbali ya ngozi hutibika pia kwa kutumia mti huu wa mwarobaini.

Kwa kutibu magonjwa hayo na magonjwa mengineyo unachotakiwa kufanya:

Chemsha majani ya mti wa mwarobaini kwa muda wa dakika kumi tano,  baadae acha mchanganyiko huo upoe, kisha chuja kwa ajili ya matumizi. Unaweza ukanywa mchanganyiko huu asubuhi na jioni. Kwa kiwango cha kikombe kimoja cha chai. Kikombe kimoja asubuhi na kingine jioni.

MAYAI YASIPOIVA NI HATARI

Mayai Yasipoiva Ni Hatari

Mayai ni moja ya vyakula vyenye viini lishe muhimu kwa ajili ya afya ya mwili wa binadamu. Kwa kawaida mayai kabla ya kuliwa, huandaliwa kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchemshwa, kukaangwa au kuchanganywa na vyakula vingine kama vipande vya viazi mviringo ambavyo ni maarufu kwa jina la chips.

Pia, kuna baadhi ya watu wanaopendelea kula mayai mabichi kama dawa ya tiba mbadala, kwa ajili ya kulainisha sauti na wengine hupendelea kula mayai ya kukaanga ambayo hayakukaushwa vizuri.
Ukitembelea migahawa mingi utabaini kuwa watu wanakuwa na mitazamo tofauti na wanavyopenda kula mayai.

Mfano kuna wanaoagiza watengenezewe mayai kwa mtindo unaojulikana kama ‘macho ya ng’ombe.’ Ukiagiza namna hiyo, mpishi atataka kuuliza kama ni ‘macho ya ng’ombe’ ya kugeuza.

Ina maana kuwa ‘macho ya ngombe’ ya kugeuzwa ni yale yanayoivishwa pande zote lakini yale ambayo siyo ya kugeuza, huwa linaiva nusu. Upande mmoja unabaki ukiwa mbichi, na ndiyo raha ya baadhi ya watu.

Hata ukienda kwa wakaanga chipsi, utakuta wanawauliza wateja wao kama wanapokaanga na mayai wakaushe au wasikaushe. Hii inaashiria kuna watu wanataka wale chipsi zikiwa na mayai ambayo halijaiva sawasawa.

Kuna watu wengine wanaamini kwamba kula mayai mabichi kunafanya sauti inakuwa nyororo, hivyo wale waimbaji huwalazimu kufanya hivyo ili kufanya nyimbo zao zivutie.

Si hivyo tu, kuna baadhi ya watu huamini pia dawa ya kikohozi ni kunywa yai bichi lililochanganywa na asali. Hizi ni imani ambazo zimejengeka kwenye jamii na watu hufanya hivyo ili kufikia malengo waliyokusudia.

Katika siku za karibuni, imevuma kuwa mayai ya kwale yanatibu magonjwa sugu kama vile kisukari, shinikizo la damu, saratani na kifua.

Katika mpango huo, wanapendekeza wahusika kula mayai mabichi ya kwale tena kwa kutafuna hadi kaka lake, yaani ganda la nje.

Hali hii imesababisha biashara ya mayai ya kwale kuwa kubwa na hata wafugaji wameongezeka mara dufu.

Tuesday, March 21, 2017

TUMIA TANGO KWA FAIDA ZIFUATAZO

Tumia Tango Kwa faida zifuatazo

Leo katika makala hii afya tujifunze  faida za Tango katika miili yetu, ikiwa watu wengi tunakula bila kujua faida zake katika maisha ya kila siku. Hivyo nakusihi uambatane nami mwanzo mpaka mwisho wa makala haya kwani naamini utakochokisoma hapa kitakwenda kukusaidia.

Zifuatazo ndizo faida za tango:
1. Tango ni chanzo kizuri cha vitamin B. Ambayo husaidia kwa kiwango kikubwa katika kusafisha figo. Na kuondoa sumu zote zilizomo mwilini.

2. Tango husaidia kuongeza maji katika mwili wa mwanadamu, kwani asilimia 95 ya tango ni maji, huku tukizingatia ya kwamba asilimia 75 ya mwili wa mwanadamu ni maji,  ambapo maji hayo ni chanzo kikuu cha usafirishaji wa chakula na damu katika mwili wa mwanadamu. Hivyo unashauriwa utumie kwa wingi tunda hili.

3. Tango pia hutumika kwenye matunzo ya ngozi/urembo ambapo tunda hili lina kiwango kikubwa cha silicon na sulfur ambazo husaidia ukuwaji wa nywele.

4. Tango lina virutubisho kama lariciresinol, pinoresinol na secoisalariciresinol ambavyo kulingana na tafiti mbali mbali za magonjwa ya kansa husaidia kupunguza aina mbali mbali za kansa hasa kansa ya matiti.

5. Kwa wale ambao wana matatizo ya kinywa hasa harafu wataalamu wanasema ya kwamba tango husaidia kuondoa harufu mbaya kinywani.

7.Tango husaidia wagonjwa wa kisukarikwani tango lina hormone ambayo huhitajika kwenye chembechembe za kongosho (pancreatic cells) ilikuweza kutengeneza insulin ambayo husaidia kudhibiti kiwango cha sukari kwenye mwili hivyo kuwasaidia wagonjwa wa kisukari. Pia watafiti wamegundua kuwa kuna kirutubisho kiitwacho sterol kilichopo kwenye tango ambacho husaidia kupunguza mafuta kwenye mishipa ya damu.

8. Kutokana na maji na virutubisho vilivyopo kwenye tango, tunda hili husaidia kupunguza homa pale inapopanda.

Cha msingi na cha kuzingatia ni kwamba kula matunda mara kwa mara kwani yana saidia sana katika afya. Endelea kutembelea muugwana blog kwa makala kama hizi.

FORBES: MABILIONEA 25 MATAJIRI AFRIKA 2017

Forbes: Mabilionea 25 matajiri zaidi Afrika 2017

Mfanyabiashara kutoka Nigeria Aliko Dangote bado ndiye mtu tajiri zaidi barani Afrika kwa mujibu wa orodha ya mabilionea mwaka 2017 iliyoandaliwa na jarida la Forbes.

Utajiri wa Dangote unakadiriwa kuwa jumla ya $12.2 bilioni.
Kuna mabilionea (wa Dola) 25 mwaka huu barani Afrika, mmoja juu ya 24 waliokuwepo mwaka jana.

Wafanyabiasha kutoka Nigeria Femi Otedola na Abdulsamad Rabiu hawakufanikiwa kuingia kwenye orodha hiyo mwaka huu.

Mtanzania Mohammed Dewji bado ndiye bilionea wa umri mdogo zaidi Afrika, utajiri wake ukikadiriwa kuwa $1.09 bilioni.

Isabel dos Santos kutoka Angola na mfanyabiashara wa mafuta Folorunsho Alakija kutoka Nigeria ndiye mabilionea wanawake pekee katika orodha hiyo mwaka huu.

Bw Dangote Dangote, ndiye mwanzilishi na mwenyekiti wa kampuni ya Dangote Cement inayoongoza kwa kuzalisha saruji Afrika. Anamiliki asilimia 90 ya hisa za kampuni hiyo.
Dangote Cement huzalisha tani 44 milioni za saruji kila mwaka na imepanga kuongeza uzalishaji kwa asilimia 33 kufikia 2020.

Dangote pia anamiliki hisa katika kampuni za chumvi, sukari na unga.
Mohammed Dewji ni afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya METL iliyoanzishwa na babake miaka ya 1970. Kampuni hiyo huhusika katika biashara ya nguo, unga, vinywaji na mafuta. Kampuni hiyo huendesha shughuli zake katika zaidi ya mataifa sita barani Afrika.

Mabilionea 25 wa Afrika mwaka 2017:

1. Aliko Dangote, Nigeria

    Utajiri: $12.2 bilioni

2. Nicky Oppenheimer, Afrika Kusini

    Utajiri: $7 bilioni

3. Mike Adenuga, Nigeria

   Utajiri: $6.1 bilioni

4. Johann Rupert, Afrika Kusini

   Utajiri: $6.3 bilioni

5. Nassef Sawiris, Misri

   Utajiri: $6.2 bilioni

6. Christoffel Wiese, Afrika Kusini

    Utajiri: $5.9 bilioni

7. Nathan Kirsch, Swaziland

    Utajiri: $3.9 bilioni

8. Naguib Sawiris, Misri

    Utajiri: $3.8 bilioni

9. Isabel dos Santos, Angola

    Utajiri: $3.1 bilioni

10. Issad Rebrab, Algeria

     Utajiri: $3 bilioni

11. Mohamed Mansour, Misri

      Utajiri: $2.7 bilioni

12. Koos Bekker, Afrika Kusini

      Utajiri: $2.1 bilioni

13. Allan Gray, Afrika Kusini

      Utajiri: $1.99 bilioni

14. Othman Benjelloun, Morocco

      Utajiri: $1.9 bilioni

15. Mohamed Al Fayed, Misri

      Utajiri: $1.82 bilioni

16. Patrice Motsepe, Afrika Kusini

      Utajiri: $1.81 bilioni

17. Yasseen Mansour, Misri

      Utajiri: $1.76 bilioni

18. Folorunsho Alakija, Nigeria

      Utajiri: $1.61 bilioni

19. Aziz Akhannouch, Morocco

     Utajiri: $1.58 bilioni

20. Mohammed Dewji, Tanzania

      Utajiri: $1.4 bilioni

21. Stephen Saad, Afrika Kusini

      Utajiri: $1.21 bilioni

22. Youssef Mansour, Misri

      Utajiri: $1.15 bilioni

23. Onsi Sawiris, Misri

      Utajiri: $1.14 bilioni

24. Anas Sefrioui, Misri

     Utajiri: $1.06 bilioni

25. Jannie Mouton, Afrika Kusini

      Utajiri: $1 bilioni


UFARANSA :WAZIRI AJIUZULU

Ufaransa:Waziri ajiuzulu

Waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa,Bruno Le Roux, amejiuzulu, baada ya kuibuka shutuma kuwa aliwaajiri binti zake wawili kuwa wasaidizi wa bunge wakiwa wanafunzi.

Waendesha mashtaka walifanya uchunguzi wa awali kuhusu mikataba yenye thamani ya karibu dola elfu sitini ambazo bwana Le Roux aliwapa binti zake kati ya mwaka 2009 na mwaka 2016.

Amesema hakuna sheria ya bunge iliyokiukwa na watoto wake walifanya kazi kwa uhalali, lakini hakutaka kuwa kikwazo kwa Serikali.

Wakati huohuo, uchunguzi kama huo umeendelea kufanyika dhidi ya mgombea urais kutoka chama cha Conservative Francois Fillon, ambaye anashutumiwa kufanya udanganyifu.

Fillon amekana kuajiri familia yake na kuwalipa mishahara minono, kashfa ambayo imetia dosari mchakato wake wa kuwania urais

KUNDI LA HEZBOLLAH LADAIWA KUMUUA KAMANDA WAKE

Kundi la Hezbollah ladaiwa kumuua kamanda wake

Afisa mkuu wa jeshi la Israel ameongeza uzito katika vyombo vya habari vya Kiarabu kwamba kundi la wapiganaji wa Hezbollah lilihusika katika mauaji ya kamanda wake nchini Syria 2016.

Luteni jenerali Gadi Eisenkot alisema kuwa idara ya ujasusi ya Israel pia ilibaini kwamba Mustafa Amine Badreddine aliuliwa na wapiganaji wake.

Aliuawa katika mlipuko karibu na Damscus ambapo kundi la wapiganaji la madhehebu ya kishia lililaumu wapiganaji wenye itikadi kali wa Sunni.

Badreddine aliaminika kuendesha operesheni zake nchini Syria tangu 2011.

Hezbollah linahusishwa pakubwa katika vita vya wenye kwa wenyewe nchini humo, likiwa limesambaza maelfu ya wapiganaji ili kumuunga mkono rais Bashar al-Asaad.

Mapema mwezi huu, kituo cha habari cha al-Arabia kilisema kuwa uchunguzi wake mwezi huu kuhusu mauji ya Bedraddine ulibaini kwamba kamanda huyo aliuawa kutokana na agizo la Hassan Nasrallah.

Ripoti hiyo inasema kuwa Hassan Nasrallah alishinikizwa kumuua Bedraddine na meja jenerali Qasema Soleiman,kiongozi wa walinzi wa jeshi la Iran.

Monday, March 20, 2017

HIKI NDICHO CHANZO CHA UGONJWA WA MABUSHA

Hiki ndicho chanzo cha Ugonjwa wa Mabusha

Ngiri nyingine ni ya Mshipa wa Kushuka ni hii hapa Mabusha kwa lugha ya kiswahilBusha ni hali ya kujaa maji kwenye mfuko wa pumbu.

Hali hii hutokea kunapokuwa na mkusanyiko wa maji kati ya tabaka mbili za utando unaozunguka korodani. Inakadiriwa kuwa karibu asilimia moja ya wanaume wote kote duniani huathiriwa na tatizo hili.

Ifahamike pia kuwa, tatizo la mabusha halitokei kwa wanaume watu wazima tu. Watoto wa kiume hususani katika mwaka wa kwanza (infants) pia ni waathirika wakuu wa tatizo hili.

Kwa kawaida busha halina maumivu na wala kuleta madhara, isipokuwa kama litapata uambukizi kwa sababu nyingine yeyote ile, hali inayowafanya wengi wa waathirika, kuwa wagumu kutafuta ufumbuzi wa tiba.

Hata hivyo, ni vyema kama mtu ana uvimbe wowote kwenye pumbu zake, kutafuta msaada wa kitabibu ili kuweza kuondoa uwezekano wa kuwepo kwa magonjwa mengine ya sehemu za siri kama vile saratani ya korodani (testicular cancer) n.k.

  Busha husababishwa na nini? Sababu za kutokea kwa busha hutofautiana kati ya watoto wa kiume na wanaume watu wazima.

Kwa watoto wa kiume Kwa watoto wa kiume, busha huweza kuanza kutokea kipindi cha ujauzito.

Wakati wa ujauzito, korodani za mtoto wa kiume huwa kwenye tumbo lake kabla ya kushuka taratibu kuelekea kwenye mapumbu.

 Wakati wa ushukaji huo, kifuko kinachozunguka korodani kinachoitwa processus vaginalis hushuka sambamba na kurodani hizo na kufanya korodani kuzungukwa na maji.

Kwa kawaida, ndani ya muda wa mwaka mmoja, kifuko hiki hufunga na maji hayo yanayozunguka korodani yote hufyonzwa na kurudishwa kwenye tumbo la mtoto.

Iwapo baada ya kifuko kufunga na maji yaliyomo kushindwa kufyonzwa kurudishwa kwenye tumbo la mtoto, mtoto hupata busha lijulikanalo kitaalamu kama busha lisilo na mawasiliano (non-communicating hydrocele).

Hali kadhalika, wakati mwingine inawezekana kifuko kikashindwa kufunga na hivyo maji yakaendelea kujaa ndani ya kifuko kuzunguka korodani.

Aina hii ya busha kwa watoto ujulikana kama busha lenye mawasiliano (communicating hydrocele). Kwa wanaume watu wazima Kwa wanaume watu wazima.

Busha husababishwa na mambo makuu mawili:

1. kitendo chochote kinachochochea tando zinazozunguka korodani kuzalisha maji kwa wingi kuliko kawaida.

2. Kupungua kwa ufyonzaji wa maji yanayozunguka korodani kwa sababu ya kuziba kwa mirija ya lymph (blockage of scrotal lymphatic system) au kuziba kwa mishipa ya damu inayosafirisha damu kutoka kwenye pumbu kwenda sehemu nyingine za mwili (blockage of scrotal venous system)

Ongezeko la uzalishaji wa maji linaweza kutokana na

Maambukizi au/na majeraha katika korodani (testicular inflammation auorchitis) Maambukizi katika mshipa ujulikanao kama epididymis yanayoweza kusababishwa na kifua kikuu (tuberculosis) cha makende,Maambukizi yanayo sababishwa na vimelea wa filaria (filariasis) wanao sababishwa na kuumwa na mbu aina ya Culex.Kujinyonga kwa korodani (testicular torsion) kunakoweza kuzifanya korodani kutenda kazi zaidi ya kiwango chake (hyperactive testis).Uvimbe katika korodani (testicular tumors) ambao husababisha uzalishaji wa maji kupita kiasi.Kupungua kwa ufyonzaji wa maji hutokana na Kufanyiwa upasuaji kipindi cha siku za nyuma katika eneo la kinena, au operesheni ya upandikizaji figo ambazo zinaweza kuathiri mfumo wa lymph na vena na hivyo kupunguza ufyonzaji wa maji kutoka kwenye mapumbu. Kuwahi kufanyiwa tiba ya mionzi kipindi cha nyuma nayo uhusishwa na kutokea kwa busha. Kwa hapa kwetu Tanzania, kung’atwa na mbu aina ya Culex anayeeneza vimelea vya filaria kunaelezwa kuwa sababu kuu mojawapo inayopelekea kuwepo kwa tatizo la mabusha na matende hususani maeneo ya Pwani na mwambao. 

Dalili za busha Katika hatua za awali,

busha huwa halina dalili zozote (asymptomatic).

Hata hivyo, baada ya muda fulani, mapumbu hujaa na uvimbe huweza kuonekana hata kwa nje. Kwa kadiri uvimbe unavyozidi kuongezeka, ndivyo dalili zingine uzidi kuonekana.

JE WAJUA ASILI YA KIDUKU

JE WAJUA ASILI YA KIDUKU?

Wengi wanapenda kucheza au kuona wengine wakicheza KIDUKU! Lakini wengi wao hawafahamu asili na chimbuko la kiduku hapa Tanzania!

Kwa kifupi ni kwamba ASILI YA KIDUKU NI NIGERIA! kiduku ni aina fulani ya ngoma inayochezwa nchini Nigeria,

Hivyo kiduku kimefika Tanzania kupitia filamu za kinigeria!

Filamu ya 'Ola' ilyotoka mwaka 2006 ndo kichochezi halisi cha style ya kiduku nchini kwani baada ya filamu ya Olakusambaa nchini Tanzania ndipo kiduku kilipoibuka na kuenea nchini Tanzania!

JINSI YA KUPUNGUZA UZITO KWA KUTUMIA SALADI

Ulaji saladi ya spinachi, matunda ya apple na parachichi unaweza kumsaidia mtu kuwa na uzito unaotakiwa kiafya.

Kabla mtu hajaanza kula mlo wake wa asubuhi, mchana au usiku anashauriwa aanze na mboga za majani za spinachi au aina nyingine.  Ulaji wa aina hii unamwezesha mtu kula kidogo vyakula vyenye wanga, sukari au mafuta ambavyo vinasababisha kuongezeka uzito na unene.

Saladi ya mboga za majani hujaza tumbo na kumfanya mtu ajihisi ameshiba na hivyo kuzuia tabia ya kutamani kula hasa vyakula vya wanga au sukari.  Mboga za majani za spinachi pia, zina kirutubisho kinachoitwa thylakoids, ambacho kinachochea mwili kuzalisha homoni inayopunguza hamu ya mtu kutaka kula hasa vyakula vyenye sukari.

Kuhusu matunda ya apple, kwa siku mtu akila tunda moja ni jambo zuri.  Matunda ya apple yana maji na nyuzi lishe ambazo zinalifanya tumbo kujisikia limeshiba.  Matunda ya epo pia yana kirutubisho cha pectin, ambacho kinakifanya chakula kilichomo tumboni kusagwa kwa muda mrefu na kumfanya mtu kujisikia ameshiba.

Mtu akila tunda zima la epo (siyo juisi), kabla ya mlo atajisikia hali ya kushiba na hivyo atakula kidogo chakula cha wanga au sukari.
Kwa upande wa matunda ya parachichi, kula nusu ya tunda hilo kwa siku kunaupa mwili mafuta bora kiafya na nyuzi lishe ambazo zinamfanya mtu ajisikie ameshiba muda mwingi na kutokutamani chakula mara kwa mara.

Anachopaswa kufahamu mtu ni kwamba kula vyakula vya wanga, sukari au mafuta kwa wingi ndipo mwili unaongezeka uzito na unene kupita kiasi. 

JINSI YA KULIMA KILIMO BORA CHA MIPAPAI

Jinsi Ya Kulima Kilimo Bora Cha Mipapai

MAHITAJI
Hali ya  hewa inayofaa kwa mipapai ni ya kitropik ambayo haina baridi kali na joto kiasi . Udongo usiotuamisha maji maji yakisimama kwa masaa 48 tu mpapai unaweza kufa, wenye ruruba ya kutosha kwa sababu mipapai haina mzizi mkuu haihiyaji udongo wenye kina kirefu, kipindi cha jua kali mpapai usiachwe zaidi ya wiki 8 bila kumwagiliwa maji kama hakuna mvua ingawa wakati wa mapapai kuiva kama kuna ukame basi hii huongeza ubora wa papai ikiwamo kutooza mapema sokoni.

Mipapai ipandwe sehemu ambazo hazina upepo mwingi kwani huvunjika kirahisi, kama unashamba la mipapai itakubidi kupanda miti ya kukinga upepo kuzunguka shamba lako, miti kama miparachichi, migravilea, vibiriti (leucaena Spp) na miembe pia inafaa. Hakikisha miti ya kukinga upepo inakuwa mirefu kuzidi mipapai kwa mita 10 mpaka 20 juu zaidi.

Kuendelea kupanda mipapai kwenye shamba moja kunaweza kusababisha usugu wa magonjwa, nashauri baada ya miaka 3 – 5 ubadilishe zao hili angalau kwa msimu mmoja ili kuua mzunguko wa magonjwa.

Mipapai inaweza kuchanganganywa na miembe na mimea jamii ya michungwa, pia mazao ya msimu kama mahindi, mtama, ufuta , alizeti  na  mboga mboga yanaweza kulimwa.

Kwa kaida kwenye mipapai kuna mipapai dume, majike  na yenye jinsia zote (multiplesex / hermaphrodite) ambayo huwa na mapapai marefu zaidi, na pia kuna isiyoeleweka ambayo huwa na mapapai mafupi sana.

MBEGU

Kusanya mbegu toka kwenye mapai makubwa na yaliyo komaa na kuiva, kausha mbegu vizuri kbla ya kupanda, kama utapata mbegu za  kununua ni vizuri zaidi, baada ya kukausha hakikisha unazipanda ndani ya wiki moja.

KUOTESHA MBEGU

Kuna wanaopendelea kuotesha mbegu kwanza na kisha kuhamishia miche shambani, sehemu ya kuoteshea iandaliwe miezi miwili kabla, mbegu zioteshwe kwenye kina kati ya sentimeta 1 – 2 chini ya udongo wenye rutuba au pakiti za plastiki, kiwango bora cha joto ni sentigredi 21 – 27 na itachukua kati ya wiki 1 – 4 kwa mbegu kuota, kwenye kila pakiti weka mbegu 2 – 3. Panda mbegu zako kwenye kitalu kwa umbali wa sentimeta 3 toka shimo hadi shimo na sentimeta 15 kati ya mistari, hakikisha maji hayatuami kabisa, pia unaweza kupiga dawa ya copper oxychloride gramu moja katika lita moja ya maji ilikukinga miche yako na fangasi.

UOTESHAJI WA MOJA KWA MOJA

Kabla ya kupanda mbegu weka mchanganyiko wa majivu na mbolea ya kuku sehemu ya kupandia, mbolea husaidia ukuaji haraka na jivu husaidia kukinga mipapai na magonjwa. Panda mbegu 3 – 5 kila shimo maana miche mingine inaweza kufa kwa magonjwa, kuliwa na wadudu au ikaota dume.

KUHAMISHA MICHE TOKA KWENYE KITALU

Miche ihamishiwe shambani ikiwa na urefu wa sentimeta 20 – 40, kama udongo unatuamisha maji panda kwenye matuta yenye urefu wa sentimeta 40 – 60 mashimo yawe na ukubwa wa sentimeta 45 upana na sentimeta 30 kina na shimo lichanganywe na udongo na samadi bila kuacha kisahani cha maji, umbali ni mita 3 kwa 3 kwani mipapai inahitaji jua la kutosha.

KUPUNGUZA MIPAPAI

Baada ya miezi 3 – 5 baada ya kupanda mipapai itatoa maua na hapo jinsia ya mipapai itajulikana na mingine itabidi ipunguzwe na hasa midume, mipapai yenye jinsi zote inatakiwa isizidi asilimia 10 – 20 na midume ibaki mmoja katika kila mijike 25, mimea yenye magonjwa pia inabidi ing’olewe.

RUTUBA YA UDONGO

Weka kiasi chakilo 2 – 5 za samadi kwenye kila mpapai kwa mwaka ili kuongeza ukuaji na uzazi, mabaki ya mimea yanaweza pia kuwekwa kama matandazo na h ii ni muhimu zaidi kipindi cha kiangazi ili kuzuia unyevu usipotee.

MAGUGU

Mipapai inapopandwa tu inaweza kuwekewa matandazo kuizunguka ili kuzuia uoataji wa magugu, magugu yang’olewe yakiwa machanga na epuka kuchimbua chini sana maana mizizi ya mipapai huwa juu juu, njia nzuri ni kuweka matandazo kwenye shamba lote ili kuzuia outaji wa magugu.

UANGALIZI

Mipapai iangaliwe dhidi ya magonjwa, ing’olewe na kuchomwa au kufukiwa chini ikiwa itabainika kuwa na maonjwa, piga dawa dhidi ya magonjwa ya fangasi na virusi mara yanapoibuka ili kuongeza uzaaji nakipato chako.

Ondoa matawi yote yatakayojitokeza pembeni ya mpapai wako, na hii ifanyike mapema kabla ya tawi kuwa kubwa.

Ondoa mapapi yote ambayo yatakuwa hayakuchavuliwa vizuri na acha yale yenye afya tu

Weka miti ya kuegemea kama mpapai utazaa matunda mengi na hasa wakati wa upepo mwingi ili kuzuia mipapai isivunjike.

Mipapai ikitunzwa inaweza kuishi mika mingi, ila kwa ajili ya mazao bora ondoa mipapai na upande mingine baada ya kila miaka mitatu (3) kwani mpapai unapo kuwa mkubwa basi rutuba yote huishia kwenye mti wenyewe.

Sunday, March 19, 2017

BUASHARA NZURI AMBAYO UNAWEZA UKAIFANYA NA KUPATA FAIDA KUBWA NI HOI HAPA

Biashara Nzuri Ambayo Unaweza Ukaifanya Na Kupata Faida Kubwa Ni Hii Hapa

Habari za leo, mpenzi msomaji wa safu hii ya biashara? Nikukaribishe kwa moyo mkunjufu ili tuweze kujifunza na elimu hii ya biashara. Andaa ubogo wako ili uweze kupokea mambo muhimu ya kukusaidi kufanikiwa.

Moja ya maswali ambayo nimekuwa nikiulizwa sana na wasomaji wetu ni kwamba je, afisa mipango Benson, nifanye biashara gani ambayo itakuwa ina faida kubwa kwangu?

Kama ambavyo nimekuwa nikiulizwa mara kadha wa kadha na swali hilo tena limekuwa likijirudia. Hivyo kwa kutumia dakika chache naomba niweze kujibu swali hilo.

Jambo la msingi sana ambalo unatakiwa kulizingatia ni kwamba kila biashara ambayo unaiona machoni mwako ina faida na hasara zake, Nimeanza kwa kusema hivyo kwani watu wengi wamekuwa wakiaangalia upande mmoja tu wa kupata faida tu.

Lakini ukweli ambao unatakiwa kuujua mapema ni kwamba kabla ya kuingia katika biashara tambua ya kwamba katika biashara hiyo kuna faida na hasara, hivyo uwe tayari kubeba mambo hayo mawili pindi yatakapojitokeza.

Biashara yenye faida huanza na wazo, wazo ambalo limekuwa likitokana na mfanyabiashara kabla ya kuanza kufanya biashara husika. Wazo hilo hujengwa na misingi ya kina ya kufanya uchunguzi yakinifu juu ya biashara hiyo.

Usipofanya uchunguzi wa kutosha juu ya biashara unayotaka kuifanya ipo siku utalalamika. Ila tunashauriwa ya kwamba katika kufanya uchunguzi wa kutosha ni lazima ujikite katika kuangalia eneo ambalo utaiendesha biashara hiyo.

Wakati unangalia eneo kwa ajili ya kufanyia biashara, angalia eneo ambalo:-

Eneo linalofikika kwa urahisi.
Angalia eneo ambalo lina uwingi wa mkusanyiko mwingi wa watu tofauti tofauti.
Tafuta eneo ambalo kuna upatikaji wa huduma za kijamii, kama vile ukaribu wa benki, umeme, maji na mengineyo mengi yatakoyokusiadia kukua kibiashara.

Angalia eneo ambalo lipo karibu na wafanyabiashara wengine. Kwa mfano, kama unafanya biashara ya mashati  basi chagua eneo ambalo kuna mfanyabiashara anauza tai. Kufanya hivi kuna msaidia mteja kutopata tabu ya kuhangaika kupata bidhaa fulani.

Lakini kubwa kuliko yote ni kwamba katika kufanya uchunguzi wa eneo la kufanyia biashara ni vyema unafanya uchunguzi kwa kuangalia hasa ni yapi mahitaji ya watu.

Kisha wewe uweze kuyasogeza mahitaji hayo karibu.
Mwisho naomba ujiulize hivi, ni wapi ambapo imepanga kufanya biashara h? Na watu wana changamoto zipi nawe umekuja suluhisho lipi? Ukipata majibu hayo huo ndio utakuwa mwanzo wa kujua biashara gani italipa eneo hilo na hatimaye kupata faida.

Hivyo niseme hivi, biashara inayolipa na kutoa faida kubwa ni ile biashara ambayo umeshaifanyia uchunguzi wa kutosha na kujua soko lake liko wapi na lina ukubwa gani. Hiyo ndiyo biashara inayolipa.