Thursday, April 28, 2016

IRAQ YAWABANA AL JAZEERA KUWA WANAKIUKA UANA HABARAI

Iraq imesema Al Jazeera imekiuka kanuni za uanahabari Serikali ya Iraq imeliamuru shirika la utangazaji la Al Jazeera kufunga afisi zake mjini Baghdad.

Wanahabari wa shirika hilo pia wamepigwa marufuku kukusanya habari nchini humo. Maafisa wa serikali wanasema shirika hilo la utangazaji limekuwa likikiuka kanuni za uanahabari, ambazo miongoni mwa mengine zinazuia mashirika ya habari kuangazia makundi ya waasi.

Shirika la Al Jazeera limesema limeshangazwa sana na hatua hiyo na limekanusha kuvunja kanuni zozote za kitaaluma.

No comments:

Post a Comment