Thursday, April 28, 2016

TRUMP KASHINDA TENA MAJIMBO MATANO MAREKANI

Trump amesema kwa sasa yeye ni kama "mgombea mteule" Donald Trump ameshinda mchujo wa kuteua mgombea urais wa chama cha Republican katika majimbo matano ya Marekani yaliyopiga kura Jumanne.

Mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton ameshinda majimbo manne kati ya matano yaliyoshiriki mchujo.

Baada ya matokeo kubainika, Bw Trump alijitangaza kuwa “mgombea mteule” wa Republican. Ushindi wake Connecticut, Delaware, Maryland, Pennsylvania na Rhode Island unamfanya kukaribia sana kutimiza idadi ya wajumbe inayohitajika kumhakikishia ushindi kabla ya kuandaliwa kwa mkutano mkuu wa chama hicho wa kuidhinisha mgombea Julai.

Upande wa Democratic, Bi Clinton amenyimwa ushindi kamili na Bernie Sanders ambaye ameshinda katika jimbo la Rhode Island.

No comments:

Post a Comment