Friday, April 29, 2016

TANESCO KUZINDUA HUDUMA KWA NJIA YA MTANDAO

Shirika la Umeme nchini Tanzania TANESCO kwa kushirikiana na Tume ya Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania COSTEC imezindua mfumo uliopewa jina la TANESCO HUDUMA mfumo utakaowawezesha watumiaji wa huduma za Tanesco kuwasiliana moja kwa moja na mtoa huduma wa shirika na kutoa taarifa za matatizo ya umeme.

Shirika la Umeme nchini Tanzania TANESCO kwa kushirikiana na Tume ya Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania COSTEC imezindua mfumo uliopewa jina la TANESCO HUDUMA mfumo utakaowawezesha watumiaji wa huduma za Tanesco kuwasiliana moja kwa moja na mtoa huduma wa shirika na kutoa taarifa za matatizo ya umeme.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa mfumo huo Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco Felichesmi Mramba amesema kuwa mfumo huo utatatua matatizo ya kimawasiliano yaliyokuwa yakilalamikiwa sana hapo awali kwani mteja ataweza kupata suluhisho la matatizo yake haraka zaidi.kupitia simu ya mkononi.

Kwa kuanzia mfumo huo utafanyiwa majaribio katika kanda ya Kinondoni Mashariki na baadae utasambaa katika maeneo mengine ya jiji la Dar es salaam na baadae kuenea Tanzania nzima.

No comments:

Post a Comment