Monday, February 20, 2017

Vita dhidi ya dawa za Kulevya Waathirika wajitokeza kwa wingi kupata dawa ya Methadone

Vita dhidi ya dawa za kulevya inayoendelea imeanza kuzaa matunda baada ya idadi ya waathirika wa dawa hizo kujitokeza kwa wingi kwenye clinic za waathirika wa dawa za kulevya zinapopatikana dawa za METHADONE.

Hata hivyo changamoto iliyopo kwa vituo hivyo inadaiwa kuwa ni uwezo mdogo wa kuhudumia idadi hiyo kubwa ya waathirika inayozidi kuongezeka siku hadi siku nchini kote hali ambayo inatoa chanagmoto kwa mamlaka husika kuangalia namna ya kujenga uwezo kwa vituo kama hivyo ili viweze kutoa huduma kwa waathirika .

Katika mahojiano maalum na Channel Ten Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni Dr Aziz Msuya amesema kuwa vituo vya vya matibabu ambavyo ni vitatu tu kwa nchi nzima ni Kliniki ya METHADONE ya Muhimbili, Mwanyamala na Temeke hali ambayo bado ni kikwazo katika kuwasaidia waathirika wa dawa za kulevya walioamua kuacha matumizi ya dawa hizo, na wameamua kwa hiyari yao kwenda kwenye vituo hivyo kupata matibabu.

Wakielezea madhara ya dawa za kulevya kwa watumiaji wa dawa hizo Mganga Mkuu Manispaa ya Kinondoni pamoja na msimamizi wa kituo cha kuwasaidia waathirika hao katika Hospitali ya Mwananyamala wanasema.

Channel ten imefanikiwa kuzungumza na baadhi ya waathirika wa dawa za kulevya ambao tayari wameshaanza kupata matibabu kwenye vituo hivyo.






No comments:

Post a Comment