Wednesday, July 6, 2016

BEI YA MAFUTA YA PETROL YAPANDA

   Mmamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji (EWURA) imetangaza bei ya kikomo cha mafuta huku bei ikiongezeka maradufu kwa watumiaji wa mafuta ya petrol.

   Mmamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji (EWURA) imetangaza bei ya kikomo cha mafuta huku bei ikiongezeka maradufu kwa watumiaji wa mafuta ya petrol. Bei mpya elekezi zilizotolewa jana na mamlaka hiyo zinaonesha kuwa dizeli imeongezeka kwa shilingi 88 kwa lita ikifuatiwa na mafuta ya taa kwa shilingi 80 kwa lita wakati petrol ikiongezeka kwa shilingi 23.

     Taarifa ya mamlaka hiyo imesema kuanzia leo wakazi Dar es Salaam watakuwa wakinunua petrol kwa bei isiyozidi shilingi 1888 dizeli 1720 na mafuta ya taa 1687.

    
    Mkurugenzi wa EWURA Bw. Felix Ngamlagosi alisema kiasi kikubwa cha mabadiliko hayo ya bei za mafuta katika soko la ndani yametokana na kuendelea kupanda kwa bei za mafuta katika soko la dunia.

No comments:

Post a Comment