Msanii wa muziki wa dansi, sanaa ya jukwaani (theatre performances), mwandishi wa vitabu vya mashairi na hadithi zenye mafunzo,amewataka watanzania kuepuka uhasama kwani uchaguzi umealizika na kinachotakiwa ni wao kujikita kwenye shughuli za ujenzi Mpoto ameyasema hayo
alipokuwa akishiriki katika kipindi cha Supa Mix kinachorushwa na East Afrika Radio Jijini Dar es salaam wakati akishiriki usiku wa mapinduzi ambao umelenga vipindi vyote kuwa na watangazaji wenza katika vipindi vyote vya redio.
Hakuna haja ya kuwa na uhasama , wananchi wanatakiwa washikamane ili kuchapa kazi na kuleta maendeleo ya taifa kwani uchaguzi umemalizika. Mrisho pamoja na kuimba nyimbo zake zenye nasaha kwa jamii pia amewataka madereva bodaboda kuheshimu kazini zao kwani ndizo zinawaingizia kipato.
''Kuna baadhi ya bodaboda wapo kama wameingiliwa na pepo, yani ukiwakuta hawathamini kazi yao wachafu na hii inatokana na wengi kupata bodaboda na kuingia mtaani bila mafunzo yoyote''amesema Mpoto.
No comments:
Post a Comment