Benki ya dunia imesisitiza nia yake ya kuendelea kuimarisha ofisi ya takwimu nchini NBS ili iwe na uwezo wa kuisaidia serikali kupunguza gharama za utafutaji na uhifadhi wa takwimu mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Nia ya Benki ya dunia ni kuijengea uwezo taasisi hiyo kukusanya takwimu ili kufikia maendeleo na kulingana na dira ya taifa ya mwaka 2025 ambapo itatoa dola milioni 2.
Mkurugenzi mkazi wa benki ya dunia, kwa Tanzania,Burundi, Malawi na Somalia BELLA BIRD ametoa kauli hiyo alipofanya ziara kwenye ofisi kuu ya takwimu ya taifa ambapo amesema pamoja na benki hiyo kusaidia ofisi ya takwimu ya taifa, msaada huo ulenge kutoa hamasa ya uchapaji kazi itakayoisaidia nchi kufikia malengo ya kutokomeza umaskini kama dunia ilivyokubaliana ifikapo mwaka 2020.
Mkurugenzi mkuu wa ofisi ya taifa ya takwimu,Dk.ALIBINA CHUWA, kwa niaba ya serikali ameshukuru kwa msaada huo utakaowawezesha kuharakisha juhudi za ofisi hiyo za kutoa takwimu sahihi kwa ajili ya maendeleo ya taifa katika mradi wa uboreshaji na uimarishaji takwimu nchini, yaani TANZANIA STATISTICAL MASTER PLAN ambao awamu ya kwanza itakamilika mwezi juni mwaka 2018.
No comments:
Post a Comment