Waliokuwa wafanyakazi wa mkataba wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA ambao ajira zao zilisitishwa wamekusanyika katika ofisi za mamlaka hiyo Kinondoni jijini Dar es salaam kushinikiza uongozi kuwalipa stahiki zao ikiwemo
mishahara ya miezi mitatu ambayo wanadai hawajalipwa pamoja na fidia ya usitishwaji wa mkataba Wakizungumza na Channel Ten iliyofika katika ofisi hizo wafanyakazi hao wameendeleza malalamiko yao dhidi ya mamlaka hiyo madai ya kufanya uamuzi ghafla wa kusitisha mikataba yao na kuutaka uongozi kuwalipa stahiki zao Aidha wameiomba serikali kuangalia upya na kuingilia kati usitishwaji wa mkataba huo uliofanywa na NIDA kutokana na waathirika wengi kuwa ni vijana.
Channel Ten hata hivyo haikuweza kufanikiwa kuzungumza na uongozi wa NIDA ili kupata ufafanuzi kuhusu malalamiko hayo baada ya kuelezwa wahusika wapo kwenye kikao
No comments:
Post a Comment