Sunday, May 29, 2016

WANAJESHI 5 WA UKRAIN WAUAWA MASHARIKI MWA NCHI

  Wanajeshi wa Ukrain Jeshi la Ukrain linasema kuwa wanajeshi watano wameuawa na wengine wanne kujeruhiwa kwa muda wa saa 24 zilizopita wakati wa mapigano na waasi wanaoiunga mkono Urusi mashariki mwa nchi hiyo.

   Hiyo ndiyo idadi ya pili ya vifo vingi vya kila siku vinavyo wakumba wanajeshi wa Ukrain Kila upande unamlaumu mwingine kwa kukiuka usitishwaji mapigano uliotiwa sahihi mwezi Februari mwaka uliopita.

    Karibu watu 9000 wanaripotiwa kuuawa kwenye mzozo huo ambao ulifuatia hatua ya Urusi ya kuimega rasi ya Crimea mwaka 2014

No comments:

Post a Comment