Friday, May 27, 2016

SERIKALI VUNJENI BODI YA SUMATRA -MBUNGE MTOLEA

  Mbunge wa Temeke Jijini Dar es salaam Abdallah Mtolea (CUF) ameitaka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuivunja bodi ya SUMATRA kwa kutosimamia sheria inayotaka watanzania theluthi mbili kuajiriwa wakati meli zinapotia nanga bandarini.

    Mtolea amebainisha Bungeni kwamba watu wanaofanya kazi katika meli nyingi zinazoingia nchini siyo watanzania ambapo sheria inataka watanzania theluthi mbili waweze kuajiriwa meli zinapoingia nchini, hivyo kwa kuwa jukumu hilo ni la SUMATRA na imeshindwa kusimamia sheria hiyo bodi yake ivunjwe na kuwekwa watendaji watakaosimamia sheria ili watanzania waweze kunufaika na ajira.

    Aijibu swali hilo Naibu Wazirin wa Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Edwin Ngonyani amesema kwamba ni kweli kuna malalamiko kutoka kwa mabaharia wengi pamoja na wafanyakazi wa meli juu ya ajira hizo ila sheria hiyo kuna namna inatafsiriwa vibaya.

     Naibu Waziri Ngonyani amesema kwamba serikali itapitia upya sheria hiyo ili iweze kutoa nafasi kwa pande zote mbili.

No comments:

Post a Comment