Friday, May 27, 2016

MADEREVA WA NWENDO KASI WAOMBA MIKATABA IWEKWE WAZI

   Mapema jana Madereva wa mabasi yaendayo haraka jijini dar es salaam walimwomba mwajiri wao kuweka wazi juu ya mikataba yao kutokana na jambo hilo kutotekelezwa kama walivyokusudia jambo ambalo linawatia wasiwasi.

   Wakizungumza na channel ten kwa masharti ya kutotajwa majina yao wala kupigwa picha wamesema tangu waanze kazi wamekuwa wakilipwa posho shilingi elfu 10 kwa siku na wakati mwingine hawapewi, huku suala la mishahara wakishindwa kulitambua kutokana na kutosainishwa mikataba ya ajira zao.

   Channel ten imemtafuta mwajiri wa madereva hao UDA-RT ambapo mkurugenzi mtendaji wake David Mgwassa ametolea ufafanuzi suala hilo kuwa hali hiyo imetokana na kutokamilika kwa baadhi ya masuala ikiwemo kufunguliwa kwa akaunti benki kuu na vibali ambavyo endapo vitapatikana zoezi la kusainishwa mikataba yao litafanyika mara moja.

No comments:

Post a Comment