Sunday, May 29, 2016

IRAN HAITAPELEKA RAIA WAKE KUHIJI MECCA

  Mecca Waziri wa utamaduni nchini Iran anasema kuwa nchi hiyo haitawatuma raia wake kwenda kuhiji mwaka huu nchini Saudi Arabia. Ali Jannati alisema kuwa sio vizuri kwa Saudi Arabia kuwawekea vizuizi raia wa Iran wanaotaka kuhiji.

    Wakati wa hija ya mwaka uliopita, mamia ya mahujaji waliuawa wengi wao raia wa Iran wakati wa kisa kibaya cha mkanyagano. Msukosuko kati ya Iran na Saudi Arabia umekuwa ukiongezeka wakati pande hizo mbili zinaunga mkono makundi tofauti yanayopigana nchini Syria na Yemen.

    Mamia ya watu waliuawa kwenye mkanyagano mwaka uliopita

No comments:

Post a Comment