Monday, May 30, 2016

CAF YARUDISHA MFUMO WA MTOANO


   Shirikisho la Soka Afrika limetaja mfumo mpya wa mashindano kuanzia mwakani, na sasa limerudisha mfumo wa mechi za mtoano kuanzia hatua ya Robo Fainali.

  Katika kikao cha Jumanne ya Mei 24, mwaka 2016 mjini Cairo, Misri; Kamati ya Mashindano ya Klabu ya CAF ilikubaliana juu ya mfumo mpya wa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho.

   Mabadiliko katika mashindano hayo mawili yalitangazwa na Rais wa CAF, Issa Hayatou katika Mkutano Mkuu wa 38 wa shirikisho hilo uliofanyika mjini Mexico City, kwamba kuanzia mwakani kutakuwan na timu 16 katika hatua ya makundi.


    Baada ya raundi za awali, timu 32 zitafuzu kuwania hatua ya 16 Bora ya mashindano yote. Watakaofuzu hatua ya 16 Bora kwa Ligi ya Mabingwa wataingizwa moja kwa moja katika makundi manne. baada ya mechi za makundi za nyumbani na ugenini,

   washindi wawili wa juu wa kila kundi wataingia Robo Fainali ambayo itaanza kuchezwa kwa mtoano hadi fainali. Klabu zitakazoongoza makundi zitaanzia ugenini katika Robo Fainali na kumalizia nyumbani.

   Katika Kombe la Shirikisho, timu 16 zitakazofuzu hatua ya makundi zitakuwa ni pamoja na zilizotolewa katika Ligi ya Mabingwa na baada ya hapo, mambo yatakwenda kama yalivyopangwa kwenye Ligi ya Mabingwa.

No comments:

Post a Comment