Monday, May 30, 2016

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA NYANYA..

  FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA        NYANYA....

Hili ni tunda mashuhuri na lenye virutubisho ambalo kwa kawaida hutumika kama mbogamboga.

Kwa wastani, watu hula takribani kilo 8 za nyanya kwa mwaka. Nyanya zina aina mbalimbali za viasili vya kurutubisha na visivyorutubisha vinavyohusiana na faida kadha wa  kadha za kiafya.

  Hii inajumuisha lycopene, vitamini C,  A na K, potasiamu, na nyuzinyuzi. Nyanya moja yenye ukubwa wa wastani inaweza  kutoa takribani nusu ya kiasi cha kila siku cha vitamini  C anachohitajika kupata mtu.

   Viasili mbalimbali vya  nyanya vinasadikika kufanya kazi pamoja kuleta  manufaa ya kiafya. Hii ni pamoja na kusaidia kujenga afya ya meno, afya  ya mifupa, afya ya ngozi, afya ya nywele, kupunguza  shinikizo la damu (PB) na kupunguza viwango vya  lehemu pamoja na kupunguza hatari ya ugonjwa wa moyo na saratani.

    Baadhi ya vionjo vya nyanya kama vile lycopene  hufyonzwa kwa wepesi mwilini pale nyanya  zinapochemshwa, iwe kwa kuzipika au kuzichemsha. Sasa huenda tunazijua faida za kula lishe kamili ya  kuleta afya ikiwa ni pamoja na kula matunda na  mbogamboga.

    Lakini wasichokijua watu wengi ni  kwamba juisi ya mbogamboga ndiyo inayosaidia  kudumisha urari (pH) muhimu wa haidrojeni ya mwili. pH ina maana ya nguvu ya haidrojeni katika mizani ya  kupimia hali-asidi ya vitu mwilini. Ili mwili ufanye kazi  vizuri na kuweza kuendelea kuishi, lazima uwe na  vikemikali vinavyolipuka na vitu vya asidi ili  kutengeneza chumvi na kutoa umajimaji wenye nguvu  ya haidrojeni (ya baina ya 7 na 7.5) na uwe na kipimo  cha haidrojeni chenye urari kamili kwa sababu saba:

1. Kuulinda mwili dhidi ya uharibifu utokanao na  chembechembe za maradhi na kuukinga na uzee wa  kabla ya wakati.

   2. Kuusaidia mwili kudumisha viwango vya lehemu  vyenye kuleta afya bora.

   3. Kuweka msukumo wa damu katika kiwango bora cha afya.

   4. Kuweka katika hali ya kawaida kikemikali cha  kusawazisha sukari ya damu (insulin) na kuzuia  ongezeko la uzito wa mwili linaloweza kuhatarisha afya.

   5. Kuuwezesha moyo kufanya kazi vizuri.

   6. Kuongeza uzalishaji wa nishati

    7. Kudumisha mfumo wa kinga ya mwili, mfumo wa  umeng’enyaji, kudumisha afya ya viungo vya mwili na mifupa

No comments:

Post a Comment