Friday, May 27, 2016

WANAWAKE WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KATIKA KUBADILI FIKRA ZA MFUMO DUME

Waziri wa nchi ofisi ya rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe Angela Kairuki amewataka wanawake kuwa mstari wa mbele katika kubadili fikra za mfumo dume na kujiendeleza kielimu kwani ndio njia pekee itakayofanikisha malengo yaliyowekwa na serikali ya kufikia uwiano wa asilimia 50 kwa 50 katika utendaji kazi kwa wanawake na wanaume kwenye sekta mbalimbali ifikapo mwaka 2030.

     Waziri Kairuki anatoa rai hiyo kwa wanawake katika uzinduzi wa katiba na mkutano mkuu wa chama cha makatibu mahususi Tanzania Tapsea ambapo amesema licha ya serikali na wadau wa maendeleo kupambana kuhakikisha mfumo dume

    unatokomezwa nchini jitihada hizo zitagonga mwamba endapo kundi hilo litashindwa kutambua umuhimu wao katika jamii kwa kujiendeleza hasa kielimu. Mhe Mary Nagu mbunge wa Hanang akizungumza katika mkutano huo amewataka wanawake kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali na kuvisajili ili viweze kufikiwa kwa urahisi na serikali huku mwenyekiti wa Tapsea Zuhura Maganga akieleza kuwa chama hicho tangu kuanzishwa kwake mwaka 2011 kimerejesha heshima na utu kwa makatibu mukhtasi ambao walikuwa wakidharaulika na kuonekana watu wa mwisho maofisini.

   Nao baadhi ya makatibu mahsusi wameelezea changamoto zinazowakabili katika utendaji wao huku wakisikitishwa na hatua ya baadhi ya wakubwa wao kuwataka au kuwadhalilisha kingono huku wakikosa mahala pa kusemea kwa hofu ya kukosa ajira.

No comments:

Post a Comment