Kahama. Tabia ya baadhi ya wakulima kuweka maji kwenye pamba kwa lengo la kuongeza uzito wakati wa kuuza imedaiwa kuwa chanzo cha upatikanaji wa mbegu zisizoota.
Hayo yamesemwa na Meneja wa Bodi ya Pamba Tanzania Kanda ya Ziwa na Magharibi, Buluma Kalidushi alipokuwa akijibu malalamiko ya wakulima wa pamba wilayani Kahama kuhusu mbegu zisizoota wanazosambaziwa na mawakala.
Kalidushi amesema swala la mbegu kutoota ni la wakulima wenyewe ambao huweka maji wakati wa kuuza pamba hali ambayo husababisha mbegu hizo kuoza na kampuni zinazouza mbegu hizo
zinaponunua pamba iliyowekwa maji bila kujua kama imeoza, husambazwa kwa wakulima na kazi ya bodi ni kuhakikisha mbegu inafika vijijini kwa wakati.
“Lakini kampuni za kuuza mbegu nazo pia zinachangia uharibifu huo kwa asilimia 50 kwa sababu zinapaswa kukagua kwanza mbegu kabla haijazinunua na kwenda kuzitolea manyoya kwa ajili ya kupandwa,” amesema Kalidushi.
No comments:
Post a Comment