Wednesday, June 22, 2016

REAL MADRID KUMRUDISHA ALVARO MORATO

    Klabu ya ​Real Madrid imetangaza kumrudisha mshambuliaji wao wa zamani Alvaro Morata hivyo atajiunga nao kwenye msimu ujao akitokea klabu ya Juventus.

      Morata mwenye umri wa miaka 23, ambaye ni mchezaji wa Hispania anayeshirikia michuano ya Euro 2016, alijiunga na Juventus mwaka 2014, baada ya misimu minne na Real Madrid kuisha.

      Alifunga magoli 27 katika miaka miwili akiwa Juventus na kuisaidia timu hiyo kushinda mataji mawili. Mshambuliaji huyo hadia sasa ameshaifungia nchi yake magoli tatu katika michuano ya Euro 2016 inayoendelea nchini Ufaransa.

No comments:

Post a Comment