Mwanza.
Wakazi wa Mtaa wa Kiloleli ‘B’ katika Kata ya Ibungilo Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, wamepinga kitendo cha mmoja wa wakazi wa eneo hilo kufunga barabara inayounganisha mtaa huo na Mtaa wa Kiloleni ‘A’ na Nyamanoro.
Jana asubuhi, mamia ya wakazi hao waliandamana hadi ofisi za Serikali za mtaa huo kuomba hatua za haraka zichukuliwe kumzuia mmiliki wakitalu namba 164LL kuendelea na ujenzi wa uzio huo ili kuepusha wananchi kuchukua hatua za kuuvunja kwa nguvu.
Wataalamu wa idira ya ardhi kutoka Manispaa ya Ilemela walio ongozwa na Mpima Ardhi wa Manisapaa hiyo, Malulu Magele walilazimika kufika eneo la tukio na kuahidi kulishughulikia suala hilo ndani ya siku saba huku wakiwaasa wananchi kuwa watulivu wakati suala hilo linashughulikiwa kisheria.
“Naomba tuwe watulivu na tuepuke kuchukua sheria mkononi kuepuka madhara wakati Serikali inashughulikia suala hili kisheria kwa faida na haki ya pande zote mbili,” amesema Malulu alipozungumza na wananchi.
No comments:
Post a Comment