Ndovu kutoka mbuga ya Nimule nchini Sudan Kusini wamekuwa wakivuka na kuingia Kaskazini mwa Uganda na kuharibu mashamba ya mahindi , mihogo , viazi na pamba Maurice Vuzi ambaye ni mwenyekiti wa wa kaunti ndogo ya Dufile, alisema kuwa ndovu hao waliharibu zaidi ya ekari 35 ya mimie siku ya Jumatatu.
Wakulima wanasema kuwa hawajui hatma yao kwa sababu kila ifikapo msimu wa kuvuna, ndovu uharibu mazao yao na wakati huu ndovu wanafika wakiwa wenge.
Mkulima moja aliliambia gazeti la Daily Monitor kuwa hili limesababisha kushuhudiwa uhaba wa chakula katika vvjiji vilivyo eneo hilo.
No comments:
Post a Comment